Bobby Duncan ambaye ni mpwa wa mchezaji wa zamani wa timu ya Liverpool Steven Gerrard ameweka wazi kwamaba wakala wake wa zamani Saif Rubie alikuwa anahatarisha kazi yake.
Duncan alikuwa mchezaji chipukizi wa kutumainiwa katika klabu ya Liverpool lakini aliondoka kwa mtindo wa kutatanisha mwaka wa 2019, baada ya Rubie kuishutumu klabu hiyo kwa ‘unyanyasaji wa kiakili’ na kutomruhusu kijana huyo kuondoka klabuni hapo.

Mshambulizi huyo alijiunga na Fiorentina muda mfupi baadaye lakini alijitahidi kufanya vyema kwenye Serie A. Baada ya kuchezea Derby, sasa anacheza ligi daraja la tatu la Uhispania akiwa na Real Balompedica Linense.

Licha ya shutuma alizotoa kwa Liverpool, Saif hivi majuzi kwa mujibu wa TalkSPORT alidai kwamba alimtaka Duncan abaki katika klabu hiyo.
Alisema: ‘Je, ninaweza kukuambia jambo fulani katika hali hiyo? Kwa kweli nilimshauri abaki Liverpool na inabidi muelewe kitu kimoja, ndicho nilichokuwa najaribu kuwaambia, kazi yangu ni kufanya kilicho bora kwa yeyote anayeniambia nimsaidie iwe mchezaji, kununuaklabu au kuuza.

‘Katika hali hiyo, unaweza kuchagua kuniamini au kutoniamini, nilifikiri kubaki kwake ndio matokeo bora zaidi. Haikukusudiwa kuwa hivyo na mwishowe ikawa mbaya kidogo na Liverpool ambayo ni bahati mbaya.’
Duncan alijibu hili kwenye twitter yake, Akisema: ‘Sikuwa na uamuzi wala kusema kwani ulichukua jukumu lako kuhatarisha kazi yangu na kumgeuza kijana wa ndani kutoka klabu yake ya utotoni na kuniacha mimi na familia yangu tukichukua vipande vyote.

“Sijazungumza mara moja juu ya hii katika “miaka 4″ kwani imekuwa kipaumbele changu kurudisha kazi yangu kwenye mstari. Lakini, bado unafikiri una haki ya kutaja jina langu kwenye kipindi cha redio mbashara”
‘Sipaswi kamwe kuamini kazi yangu mikononi mwako. Nimejifunza somo langu kali hapo. Na ninaomba tu kwamba umejifunza yako kwani inaweza kuharibu kazi kwa vijana wengine”

