Pan Yapania Kupanda Ligi Kuu

WAKITARAJIA kumenyana na Kitayosce, Uongozi wa Pan African umefunguka kuwa malengo yao kwa msimu huu ni kuhakikisha wanapata nafasi ya kupanda ligi kuu.

Pan Yapania Kupanda Ligi Kuu

Klabu hiyo ambayo inashiriki michuano ya Championship kwa msimu huu inatarajia kucheza mchezo wake wa kwanza kwenye ligi dhidi ya Kitayosce ya Tabora, Septemba 17, mwaka huu.

Akizungumzia malengo yao, Ofisa Habari wa Klabu hiyo yenye makao makuu yake Jijini Dar Es Salaam, Leen Essau alisema kuwa “Kikosi chetu kinaendelea vizuri na maandalizi ya mchezo wetu wa kwanza dhidi ya Kitayosce.

Pan Yapania Kupanda Ligi Kuu

“Timu tayari imeondoka Dar kwa ajili ya mchezo huo na mipango yetu ni kupata pointi sita katika michezo miwili ya ugenini ambayo tutaenda kucheza dhidi ya Kitayosce na Mashujaa.

“Malengo tuliyojiwekea kwa msimu huu ni kuhakikisha haturudii makosa ambayo tumeyafanya kwa msimu uliopita na kutafuta nafasi ya kushiriki ligi kuu kwa msimu ujao.”

Pan Yapania Kupanda Ligi Kuu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.