Nahodha Simba SC aahidi ushindi

NAHODHA Msaidizi wa Simba SC, Mohamed Hussein amesema kuwa Simba SC ni timu kubwa ya mataji hivyo wataenda kupambana kwenye mchezo wa kesho dhidi ya Nyasa Big Bullet.

Mchezo huo utapigwa kesho jumapili kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar huku Simba SC wakiwa na faida ya mabao 2-0 waliyopata kwenye mchezo wa kwanza wakiwa ugenini.

Nahodha Simba SC aahidi ushindi

Mohamed Hussein alisema kuwa “Kikubwa ni kuendelea kupambana ili tupate matokeo na kuingia kwenye hatua inayofuata, taratibu tutakuwa tunaelekea kwenye malengo yetu.

“Natoa shukrani zangu za dhati kwa mashabiki na tunaahidi kufanya vizuri na kupambana kwa ajili ya viongozi, mashabiki na sisi wenyewe kwani mpira ndio maisha yetu.

Nahodha Simba SC aahidi ushindi

“Kikubwa tunachozungumza tukiwa kambini ni kutengeneza kitu kimoja, utamaduni wa klabu na malengo ya klabu kwa msimu husika, Simba ni timu ya mataji lakini pia timu ya mafanikio.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.