Benjamin Sesko Anahusishwa Kusajiliwa Man Utd

Mlengwa wa Manchester United katika usajili wa majira ya kiangazi Benjamin Sesko alionyesha kile ambacho Mashetani Wekundu wanakikosa wakati alipofunga bao la ajabu kwa timu yake ya taifa ya Slovenia dhidi ya Sweden Jumanne usiku.

 

Benjamin Sesko Anahusishwa Kusajiliwa Man Utd

United ilionyesha nia ya kumtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 19 wakati wa dirisha la usajili lililopita, lakini amechagua kujiunga na RB Leipzig msimu ujao badala yake, na kwa sasa anacheza katika msimu wake wa mwisho katika klabu ya Red Bull Salzburg.

 

Benjamin Sesko Anahusishwa Kusajiliwa Man Utd

Licha ya kutofikisha miaka 20 hadi Mei ijayo, Sesko tayari amejiimarisha katika timu ya taifa ya Slovenia, na alifunga bao lake la nne kwa nchi yake kwa mtindo wa kuvutia.
Mchezo huo ukiwa haujafungana dakika ya 28, Petar Stojanovic alicheza pasi ya juu kuelekea upande wa kushoto wa eneo la hatari.

 

Benjamin Sesko Anahusishwa Kusajiliwa Man Utd

Akiikimbilia kwa kasi, Sesko alionyesha ufundi mzuri sana wa kupiga shuti bila kutuliza kwa mguu wa kushoto na kufunga goli zuri sana.

Nyota huyo anayechipukia anaendelea kuimarika na sasa amefunga katika kila mechi tatu za mwisho za kimataifa. Pia ameanza kwa kasi msimu huu akifunga mabao manne katika mechi tisa za ligi nchini Austria.

 

Benjamin Sesko Anahusishwa Kusajiliwa Man Utd

Sesko ameshiriki katika mechi zote mbili za Salzburg za UEFA, ambazo zimeshuhudia timu yake ikiwabana AC Milan na Chelsea kwa sare ya 1-1.

Anaonekana kuwa na ulimwengu miguuni mwake katika umri mdogo, na United inaweza kuwa kwenye nafasi mbaya ya kuinasa saini ya mchezaji huyo.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.