Cedric Kaze ambaye ni Kocha msaidizi wa Yanga na Mkurugenzi wa Ufundi na timu ya vijana ya klabu hiyo, amefafanua suala la ‘Unbeaten’ ambalo limekuwa likizungumzwa sana kwenye mitandao ya kijamii.

Kaze amesema kuwa Unbeaten ni matokeo tu ya mchezo na Yanga hawachezi kwa sababu ya hiyo.
“Ni kweli tuna takwimu nzuri ambayo ni heshima kwa Klabu. Lakini hatuchezi kwa sababu ya rekodi ya unbeaten, tunacheza kushinda ili tufikie malengo yetu. Kwenye mafanikio yetu hatuna malengo ya unbeaten, tuna malengo ya kutwaa mataji yaliyopo mbele yetu. Unbeaten ni matokeo sio mafanikio. Sisi tunataka mafanikio”

Kauli hii ya Kocha Cedric Kaze imekuja kutokana na klabu yake anayoifundisha kuwa na rekodi hiyo ya kutopoteza mechi yeyote kwa michezo 47 mpaka sasa, ikiwa chini ya Kocha Mkuu Nasraddine Nabi ambaye alitambulishwa klabuni hapo April 2021.
Yanga wanakabiliwa na mchezo mwingine mbele yao, dhidi ya Mbeya City ukiwa unatarajiwa kupigwa majira ya saa 12:15 jioni. Je unadhani Mbeya City wataharibu rekodi ya Unbeaten ya Yanga? Beti na kitochi Meridianbet mechi hii ina ODDS kubwa.
Je wewe hucheza Kasino Mtandaoni na umekuwa ukijiuliza ni mchezo gani rahisi na mzuri kwa ushindi? Basi Usihangaike Aviator ni rahisi zaidi kucheza na kushinda, kingine cha zaidi ni kwamba Aviator Bonanza imerudi tena Cheza zaidi ujiweke kwenye nafasi ya kushinda Samsung A23.


