Klabu ya Soka ya Ihefu fc kutoka mkoani Mbeya imefanikiwa kuiadhibu klabu ya Mtibwa Sugar kutoka mkoani Morogoro katika mchezo wa ligi kuu ya NBC mchezo ulipigwa katika dimba la Highland Estate jijini Mbeya.
Katika mchezo huo ulioonekana kua na kasi kwa pande zote mbili huku Ihefu wakionekana kuitafuta Mtibwa Sugar zaidi kwa mashambulizi ya hapa na pale, Lakini mchezo huu mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika hakuna timu iliyofanikiwa kuonalango la mwenzake.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku vijana hao kutoka mkoani Morogoro wakionekana kua na usongo zaidi kwani dakika ya 52 Ismael Mhesa alianadikia Mtibbwa bao la kuongoza, Lakini vijana kutoka jijini Mbeya kupitia kwa Joseph Mahundi dakika ya 60 akaisawazishia Ihefu bao na mchezo kua moja kwa moja.
Klabu ya Ihefu ilionekana kuamka zaidi baada ya kupata bao la kusawazisha na kutafuta bao la pili mpaka dakika 74 Obrey Chirwa akaipatia bao la pili Ihefu Fc, Na kuipa uongozi klabu hiyo katika mchezo huo.
Klabu ya Ihefu iliofanikiwa kupata bao la tatu kupitia kwa Joseph Mahundi mnamo dakika ya 88 ya mchezo na kuhakikisha klabu hiyo inavuna alama tatu muhimu kwenye mchezo huo, Na kufanikiwa kufikisha alama 17 katika msimamo wa ligi hiyo.

