Azam Yaichapa Bakora TZ Prisons Chamazi

Klabu ya Azam FC yaendeleza ushindi wake wa pili mfululizo baada ya kuichapa bakora tatu nunge timu ya Tanzania Prisons kwenye mchezo wao wa raundi ya 20 uliopigwa majira ya saa 2:30 usiku Chamazi.

 

Azam Yaichapa Bakora TZ Prisons Chamazi

Mabao hayo ya Azam yalitupiwa kimyani na Prince Dube, Sopu pamoja na Kipre Junior katika vipindi vyote vya mchezo huku Sopu akiendeleza kupachika mabao kwenye kila michezo ya hivi karibuni.

Baada ya ushindi huo sasa vijana wa Kally Ongala wamebaki nafasi yao ile ile ya tatu kwenye msimamo wakiwa wamekusanya pointi zao 43 baada ya michezo 20 waliyocheza huku Wajela jela wakiwa na pointi zao 21.

Azam Yaichapa Bakora TZ Prisons Chamazi

Tanzania Prisons wamepoteza mechi mbili mfululizo kwenye ligi hadi sasa na mchezo unaofuata watamenyana dhidi ya Ihefu ambao nao wametoka kupoteza mchezo wao wa jana.

Kituo kinachofuata kwa Azam ni dhidi ya Singida Big Stars ugenini, ambao wapo nafasi ya nne na wanatarajia kukipiga leo dhidi ya Kagera Sugar.

 

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.