Klabu ya Chelsea ina mpango wa kumuuza mchezaji wake raia wa kimataifa wa Ghana Callum Hudson Odoi nchini Italia katika klabu ya Lazio.
Callum Hudson Odoi ambaye alikua kwa mkopo kwenye klabu ya Bayern Leverkusen msimu uliomalizika na sasa klabu ya Chelsea inafanya mazungumzo na klabu ya Lazio kwajili ya kumuuza jumla mchezaji huyo.
Klabu ya Chelsea ipo kwenye mpango wa kutengeneza timu mpya ambayo itakuja kufanya vizuri siku za mbeleni, Hivo kwasasa wanaondoa wachezaji wengi ambao hawapo kwenye mipango yao ya mbeleni na hii imethibitika zaidi kwenye dirisha hili.
Odoi mchezaji ambaye ametoka kwenye akademi ya Chelsea ambapo mwanzoni alianza vizuri, Lakini alikuja kipoteza ubora wake baada ya kuandamwa na majeraha ya mara kwa mara na sasa matajiri hao wa London wanakaribia kumuuza.
Klabu ya Lazio inaelezwa kufikia hatua nzuri na Chelsea kwajili ya Odoi huku vilabu mbalimbali kutoka ndani ya ligi kuu ya Uingereza vikionesha nia, Lakini Lazio mpaka sasa ndio wanaonekana wanaweza kumtwaa mchezaji huyo kwani wamefikia pazuri kwenye mazungumzo.

