Mshambuliaji wa klabu ya Tottenham Hotspurs na timu ya taifa ya Uingereza Harry Kane anatarajiwa kua mchezaji wa klabu ya Bayern Munich baada ya vilabu hivo kufikia makubaliano.
Klabu ya Tottenham inaelezwa kukubali kiasi cha zaidi Euro milioni 100 kilichowekwa na klabu ya Bayern Munich ambapo hapo awali walikataa kiasi cha Euro Milioni 100 inaelezwa Bayern wamevuka zadi ya kiasi hicho.
Harry Kane amekua kwenye mpango wa ku9ondoka ndani ya Spurs kwa muda mrefu na akihusishwa na vilabu kadhaa ikiwemo Man United na Real Madrid, Lakini kwasasa anaelekea klabu ya Bayern Munich mabingwa wa soka nchini Ujerumani.
Klabu ya Tottenham imekua ikiweka ugumu kumuuza mchezaji huyo kwa misimu kadhaa nyuma, Lakini kwasasa wamekubali kumuuza mchezaji huyo bora kabisa klabuni hapo na akiondoka kama mfungaji wa muda wote ndani ya klabu hiyo.
Mshambuliaji Harry Kane sasa ni wazi anaiacha salama rekodi ya Alan Shearer ya ufungaji bora wa muda wote katika ligi kuu ya Uingereza, Kwani alibakisha magoli 47 kuvunja rekodi hiyo kwani Shearer ana magoli 260 na Harry Kane tayari alishafunga mabao 213.

