Kocha wa klabu ya Manchester United Erik Ten Hag amesema kua hafurahishwi na wanaomkosoa beki wa klabu hiyo Harry Maguire kwakua ni kumkosea heshima beki huyo.
Kocha Ten Hag anasema wanaomkosoa Maguire kila siku ni kumkosea heshima beki huyo kwkaua beki huyo ni mchezaji mkubwa na kitu cha ajabu sana kuona watu wananyoendelea kumkosea heshima.
Beki Harry Maguire amekua akipokea ukosoaji wa kiwango cha juu kutokana na kiwango chake ambacho amekua akikionesha siku za hivi karibuni jambo ambalo limemfanya hata mama yake mzazi kutoka kadharani na kukemea.
Kocha Ten Hag amesema beki Harry Maguire amekua akionesha kiwango kizuri vilevile ni mchezaji mkubwa na kocha huyo anasema haelewi kwanini watu wanaendelea kufanya ukosoaji wa beki huyo.
Beki Harry Maguire amekua na kipindi kigumu sana hivi karibuni kwani mashabiki wa timu zake zote mbili ambazo ni Man United na timu ya taifa ya Uingereza wote wamekua wakimkosoa kwa maneno makali jambo ambalo kocha wa klabu yake ameonesha kutofurahishwa nalo.

