Bocco amesajiliwa na JKT Tanzania kwa mkataba wa mwaka mmoja baada ya Simba kumpa mkono wa kwaheri, licha ya kwamba alipewa majukumu mengine ya kukinoa kikosi cha vijana wenye umri chini ya miaka 17.
“Ndemla na Bryson walikuwa wanacheza kwa mkopo kutoka Singida Fountain Gate kwa sasa tumewasainisha mikataba mipya kama wachezaji huru,” amesema.