Kiungo tegemeo wa Manchester City, Rodri, ameongeza moto kwenye tetesi za uhamisho baada ya kutoa majibu ya kificho kuhusu mustakabali wake klabuni hapo. Nyota huyo wa Hispania pia amekiri kuhisi kuchoshwa na kushindwa kwa timu yake kumalizia mechi vizuri msimu huu.

Real Madrid wanaripotiwa kumuweka Rodri kama kipaumbele katika mipango yao ya baadaye, wakimuona kama kiongozi bora wa kizazi kipya cha wachezaji katika dimba la Santiago Bernabéu. Akiwa ni zao la zamani la Atletico Madrid, kurejea Hispania kunaonekana kuwa chaguo lenye mvuto mkubwa kwake.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Alipoulizwa moja kwa moja kuhusu uwezekano wa kuondoka Manchester City, Rodri hakutoa jibu la wazi, jambo lililozidi kuchochea uvumi. Alisisitiza kuwa kwa sasa anaangazia msimu wake na majukumu yake na timu, huku akiacha mlango wazi kwa maamuzi ya baadaye.
Wakati huohuo, kiungo huyo ameonyesha kutoridhishwa na mwenendo wa timu yake, hasa kwenye eneo la mwisho la ushambuliaji. Baada ya sare dhidi ya West Ham, alieleza kuwa City wanakosa makali ya kufunga mabao ya kuhitimisha mechi, hali inayowagharimu pointi muhimu.

Pamoja na mkataba wake kuendelea hadi 2027, kukosekana kwa mazungumzo mapya ya kuuboresha kumeibua wasiwasi. Ikiwa hali hiyo itaendelea, mvuto wa kujiunga na Real Madrid unaweza kuwa mkubwa zaidi. Hata hivyo, kwa sasa Rodri anaelekeza nguvu zake katika mechi muhimu ya UEFA Champions League dhidi ya Real Madrid, wakihitaji kufanya miujiza kufuta kipigo cha 3-0 walichopata kwenye mchezo wa kwanza.

