FIFA Yataja Waamuzi Wa Kombe la Dunia 2026, Wanawake Sita Wajumuishwa

Shirikisho la Soka Duniani, FIFA, limetangaza orodha ya waamuzi watakaochezesha mechi za Kombe la Dunia 2026 litakalofanyika kuanzia Juni 11 hadi Julai 19, likiwajumuisha jumla ya waamuzi 52, wakiwemo wanawake sita.

FIFA Yataja Waamuzi Wa Kombe la Dunia 2026, Wanawake Sita WajumuishwaMbali na waamuzi hao wa kati, FIFA pia imeteua waamuzi wasaidizi 88 pamoja na maafisa 30 wa VAR (Video Assistant Referee), wote wakitoka katika mashirikisho sita ya soka duniani na nchi wanachama 50.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Mkuu wa idara ya waamuzi wa FIFA, Pierluigi Collina, amesema waamuzi walioteuliwa ni miongoni mwa bora zaidi duniani, wakichaguliwa baada ya kufuatiliwa kwa muda wa miaka mitatu.

FIFA Yataja Waamuzi Wa Kombe la Dunia 2026, Wanawake Sita Wajumuishwa“Waamuzi walioteuliwa ni bora zaidi duniani. Walikuwa sehemu ya kundi kubwa lililotambuliwa na kufuatiliwa kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita. Wamehudhuria semina na kuchezesha mashindano mbalimbali ya FIFA,” amesema Pierluigi Collina.

Ameongeza kuwa, “Mbali na hilo, viwango vyao vimekuwa vikifanyiwa tathmini mara kwa mara kupitia mechi za ndani na za kimataifa ili kuhakikisha ubora wao unaendelea kuimarika.”

FIFA Yataja Waamuzi Wa Kombe la Dunia 2026, Wanawake Sita WajumuishwaKombe la Dunia 2026 litakalofanyika katika nchi za United States, Canada na Mexico linatarajiwa kuwa kubwa zaidi katika historia, likihusisha timu 48 na jumla ya mechi 104, ikiwa ni ongezeko kubwa ukilinganisha na mashindano ya 2022 FIFA World Cup yaliyokuwa na timu 32 na mechi 64.

FIFA Yataja Waamuzi Wa Kombe la Dunia 2026, Wanawake Sita WajumuishwaKwa upande wa ushiriki wa wanawake, Pierluigi Collina amesema “Uteuzi wa waamuzi sita wanawake unaendeleza mwelekeo ulioanza miaka minne iliyopita huko Qatar, ambapo pia wanawake walipata nafasi ya kuchezesha mechi za Kombe la Dunia.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.