Nahodha wa Inter Miami CF, Lionel Messi, amerudi Hispania na kununua klabu ya daraja la tano ya UE Cornellà, hatua iliyothibitishwa rasmi na klabu hiyo Alhamisi. Uamuzi huo unaashiria mwanzo wa safari mpya kwa nyota huyo wa Argentina nje ya uwanja.
Kupitia taarifa yao, Cornella walisema, “Hatua hii inaonesha uhusiano wa karibu wa Messi na Barcelona pamoja na dhamira yake ya kukuza michezo na vipaji vya ndani Catalonia.” Kauli hiyo inaonesha malengo ya muda mrefu ya mchezaji huyo katika maendeleo ya soka la vijana.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Klabu hiyo imewahi kuzalisha vipaji kadhaa vikubwa akiwemo kipa wa Arsenal FC, David Raya, pamoja na mchezaji wa zamani wa Barcelona, Jordi Alba. Hata hivyo, Cornella imekuwa ikipitia kipindi kigumu baada ya kushuka daraja mara mbili mfululizo katika misimu miwili iliyopita.
Katika taarifa hiyo, klabu iliongeza kuwa, “Ujio wa Leo Messi unaashiria mwanzo wa sura mpya katika historia ya klabu, tukilenga kukuza maendeleo ya kiuchezaji na kiutawala, pamoja na kuwekeza zaidi katika vipaji.” Kauli hiyo inaonesha matarajio makubwa waliyonayo chini ya umiliki mpya.
Messi, ambaye aliibukia katika akademi ya FC Barcelona, alitumia miaka 17 katika kikosi cha kwanza na kuwa mfungaji bora wa muda wote wa klabu hiyo akiwa na mabao 672. Nyota huyo mwenye miaka 38 amewahi kueleza nia ya kurejea kuishi Catalonia baada ya kustaafu soka.
Wakati huo huo, Messi anatarajiwa kuendelea kuiongoza Argentina katika utetezi wa taji la Kombe la Dunia litakalofanyika katika nchi za Marekani, Mexico na Canada. Hatua yake inafanana na ile ya mpinzani wake mkubwa Cristiano Ronaldo, ambaye hivi karibuni alinunua asilimia 25 ya hisa katika klabu ya Hispania ya daraja la pili, UD Almería.

