Arbeloa Amtetea Kylian Mbappe Baada ya Lawama za UCL

Kocha wa Real Madrid, Alvaro Arbeloa, amejitokeza hadharani kumtetea mshambuliaji nyota Kylian Mbappe kufuatia lawama zilizomkumba baada ya kichapo cha UEFA Champions League dhidi ya Bayern Munich.

 Arbeloa Amtetea Kylian Mbappe Baada ya Lawama za UCLReal Madrid waliondoshwa kwenye mashindano hayo baada ya kupoteza kwa jumla ya mabao 6-4, huku wakichapwa 4-3 katika mchezo wa marudiano uliokuwa na ushindani mkubwa. Hali ilizidi kuwa ngumu baada ya Eduardo Camavinga kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 86, jambo lililoruhusu Bayern kufunga mabao mawili ya haraka na kuzua mjadala kuhusu mchango wa Mbappe katika ulinzi.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Akizungumza na waandishi wa habari kabla ya mchezo dhidi ya Deportivo Alaves, Arbeloa alisema, “Sina cha kumlaumu Kylian. Alikuwa katika kiwango cha juu, alifunga katika mechi zote mbili na alikuwa tishio muda wote kwa wapinzani.”

 Arbeloa Amtetea Kylian Mbappe Baada ya Lawama za UCLAliendelea kusisitiza mchango wa mchezaji huyo akisema, “Alijituma hata katika majukumu ya ulinzi na alifanya kazi kubwa sana. Nimeridhishwa kabisa na kiwango chake katika mechi hiyo.”

 Arbeloa Amtetea Kylian Mbappe Baada ya Lawama za UCLLicha ya Mbappe kufunga mabao 40 katika mashindano yote msimu huu, atalazimika kusubiri tena kutimiza ndoto yake ya kutwaa taji la UEFA Champions League. Wakati huo huo, hatma ya Arbeloa ndani ya klabu hiyo bado haijawa wazi, huku Barcelona wakiwa mbele kwa pointi tisa katika mbio za ubingwa wa La Liga.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.