Virgil van Dijk, Messi na Ronaldo -Tuzo za Fifa

Baada ya Virgil van Dijk kunyakua tuzo ya UEFA kama mchezaji wa mwaka kwa soka la wanaume, staa huyu tena ameingia kwenye hatua orodha ya 4 bora wanaowania tuzo nyingine Fifa.

Virgil van Dijk, alikuwepo pamoja na nyota wa zamani wa Real Madrid Christiano Ronaldo na Lionel Messi kwenye lala salama ya kinyang’anyiro cha tuzo za UEFA. Mastaa hawa wote wameingia pia kwenye fainali ya kinyang’anyiro cha tuzo za FIFA, -Best Fifa Footbal Award. Nyota wa Lyon Lucy Bronze naye yupo kwenye tuzo hii kama mchezaji bora wa kike.

Bosi wa Manchester City, Pep Guardiola, Jurgen Klop wa Liverpool na Mauricio Pochettino wa Tottenham Hotspurs wanachuana kutwaa tuzo ya kocha wa mwaka.

Fifa Coach 2019

Alisson Becker wa Liverpool, Marc ter Stegen wa Barcelona na Ederson Morae wa Man City wanachuana kutwaa tuzo ya golikipa bora wa mwaka -FIFA.

Goalkeeper Fifa 2019

Washindi wanatarajiwa kutangazwa Septemba 23. Inaweza kuwa shavu kwa Virgil van Dijk tena? huenda ikawa nafasi nyingine kwa staa huyu, lakini bado ana ushindani mkubwa kutoka kwa wakali Ronaldo na Messi, lolote linaweza kutokea.

Makala iliyopita
Makala ijayo

3 Komentara

    Namkubali sana,beki kisiki.

    Jibu

    Wote wakal sana

    Jibu

    Haki itendekeh

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.