Msimu wa Eredivisie 2019/20 Kufutwa au Kumalizika?

Msimu wa Ligi kuu nchini Uholanzi maarufu kama Eredivisie kimsingi umekwisha, kufuatia tamko la waziri wa nchi kupiga marufuku michezo hadi mwezi Septemba.

Shirikisho la Mpira wa Miguu la Uholanzi (KNVB) limesema linatarajia kumaliza msimu wa Eredivisie wa 2019-20 baada ya waziri mkuu wa Uholanzi, Mark Rutte kutangaza Jumanne kuwa Michezo yote ni marufuku hadi Septemba 1 kutokana na janga la virusi vya Corona.

Waziri Mkuu wa Uholanzi, Mark Rutte

Ligi Kuu ya Uholanzi imesimamishwa tangu mwezi Machi, ikiwa na michezo tisa iliyobaki kumaliza msimu na Ajax ndio anaongoza msimamo mbele ya AZ kwa tofauti ya magoli.

Kikosi cha Ajax

Ingawa ligi nyingi barani Ulaya zinafikiria kurudi mwezi Juni na michezo kufanyika bila mashabiki, Rutte amesema kwamba hata mechi zikiwa hazina mashabiki haziruhusiwa hadi mwanzoni mwa mwezi Septemba.

Kufuatia tangazo la Rutte, KNVB imetoa taarifa ikisema inatarajia kumaliza msimu wa Eredivisie na itawasiliana na UEFA ili kujua utaratibu wa kumaliza msimu.

Matokeo ya msimu mzima yanaweza kufutwa, au KNVB inaweza kuamua kumpa Ajax ubingwa kulingana na msimamo wao wa sasa wa Eredivisie

5 Komentara

    safi

    Jibu

    Big up

    Jibu

    Mmh tutakosa raha dah

    Jibu

    Habar njema sana 👍

    Jibu

    Gud news

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.