Dybala na Corona

Paulo Dybala amepima na kukutwa na virusi vya ugonjwa wa Corona kwa mara ya nne katika wiki sita, kulingana na ripoti. Mshambuliaji huyo wa Juventus alithibitishwa mnamo Machi 21 kuwa yeye na mpenzi wake, Oriana Sabatini walikuwa wameambukizwa COVID-19 baada ya vipimo vya kwanza vya ugonjwa huo.

Dybala amechukuliwa vipimo vinne katika wiki sita na bado yupo vile vile sawa na utambuzi wake wa kwanza. Nyota huyo kimataifa wa Argentina alizungumza hivi karibuni juu ya kupigana na ugonjwa huo, na kuelezea jinsi alivyokuwa akipata taabu kupumua.

“Kwa bahati nzuri tuko vizuri, siku hizi hatuna dalili yoyote,” alisema Dybala. “Nilikuwa na dalili zilizonimaliza nguvu, nilichoka haraka sana, wakati ninataka kufanya mazoezi, nilikuwa na pumzi kidogo baada ya dakika tano… Hapo ndipo tuligundua kuwa kuna kitu hakikuwa sawa na kupitia vipimo vya klabu yetu viliambiwa kwamba tulikuwa na COVID-19”.

Dybala alikuwa mmoja wa nyota watatu wa Juve kukutwa na coronavirus baada ya Dani Rugani na Blaise Matuidi kuthibitishwa kesi. Waziri Mkuu wa Italia Giuseppe Conte alisema wachezaji wataweza “kufanya mazoezi binafsi kutoka Mei 4, kwa vikundi kutoka Mei 18, kisha tutatathmini ikiwa kuna masharti ya kuruhusu msimu kukamilika.” Hivi Sasa Haijulikani ikiwa taarifa hii ya hivi karibuni kwa Dybala itaathiri uamuzi huu.

11 Komentara

    Get well soon champs

    Jibu

    Tumuombee mungu apone haraka aungane na machampion wengine

    Jibu

    Inabidi azingatie mashariti ili aweze kupona kabisa

    Jibu

    Mungu ambariki alone haraka

    Jibu

    Da! Pole yake,Mungu amponye haraka

    Jibu

    mambo yatakuwa sawa

    Jibu

    Afya kwanza Mungu akusaidie

    Jibu

    dah jembe letu ila mungu atampa wepesi atapona tu

    Jibu

    Mungu ambariki apone haraka.

    Jibu

    pole sana dybala

    Jibu

    Pole kijana

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.