Mwenyekiti wa kamati ya matibabu wa UEFA anasema michuano inaweza kuanza tena licha ya mwenzake wa FIFA kusema haipaswi kuanza kabla ya Septemba. Mwenyekiti wa kitengo cha Matibabu cha Shirikisho la Soka barani Ulaya (UEFA) Tim Meyer amesema ni jambo linalowezekana kupanga mpango wa kuanza tena ligi za soka barani humo ili kumaliza sehemu ya msimu iliyobakia.
Tim Meyer
Meyer ameeleza kwamba hatua zilizochukuliwa na zinazoendelea kuchukuliwa kwa ajili ya kupambana na Corona soka linaweza tena kuanza kuchezwa. Kauli hiyo ya mwenyekiti wa matibabu wa UEFA inakinzana na ile kauli ya mwenyekiti wa kamati ya matibabu ya FIFA Michel D’Hooge aliyotoa siku ya Jumanne akisema kuwa mpira wa miguu haupaswi kuchezwa kwa sasa angalau hadi mwishoni mwa mwezi wa nane au mwanzoni mwa mwezi wa tisa ili kuzuia kuenea kwa maambukizi mapya ya Virusi vya Corona.

Wakati huohuo mjumbe wa kamati kuu ya UEFA Lars-Christer Olsson ambaye pia ni rahisi wa Ligi ya Ulaya amesema janga la virusi vya Corona litaharibu kalenda ya soka la Kimataifa na itaathirika kwa zaidi ya miaka miwili mpaka mitatu. Lars Olsson amesema kuwa kesi ya kusubiri na kutathimini janga la Corona ni pamoja na kuangalia michuano ijayo ya Kombe la Dunia ambayo itafanyika nchini Qatar 2022.
Olsonn amesisitiza pia lazima ufanyike mpango mbadala wa kurekebisha madirisha ya Kimataifa ya majira ya kiangazi na kuangalia uwezekano wa kurekebisha ratiba ya kufuzu kwa michuano ijayo ya Kombe la Ulaya maarufu kama Euro.


Asia Abdy
Ni bora wangesubiri mpaka kuhakikisha ugonjwa umeisha wote pande za dunia maana wachezaji wanatoka pande mbalimbali za dunia
Daniel
good information thanks Meridian
David pere
Ni kitu Cha msingi ligi kurudi watu waendelee kupata burudani
SADICK
Corona imeharibu mambo mengi. Shukrani meridian kutuletea habari hii
Hamidu shabani
Ni wazo zuri.
nasra
Wasubir mpaka corona iishe kwanza
Rehema dickson
Hii habari mzuri sanaaa Asante meridian kwa taarifaa hii
Dorophina
Corona inatufanya tusi make mkwanja
Ester jackson
Asante meridian mana ugonjwa huu no wakutisha .hii njia mliotuletea in mnzuri sana
Neema hassan
Wasubiri Corona iishe af wajipange upya…
Aziza moshi
Ligi isubiri mpaka Hali itulie kabisa kwa usalama
David pers
Warudishe ligi Ila kwa mashalti ya ktokuwa na mshabiki ili burudani iendelee
Agness
Tunashuru kwa ujumbe meridian ila wasubiri corona iishe
felister
ligi zirudi lkn kusiwepo mashabik
Amani macha
Hawapaswi kukinzana wanatakiwa wawe wamoja ili soka lisonge mbele
Ernest Kimeru
Thank you Meridianbet for keeping us updated!!!!!
Emmy cleopa
Wasubir Kwanza huu ugonjwa wa corona upite ili muendelezo wa ligi uendelee
JULIANA
Wazo zuri ila kwakipindi iki Cha cov19 uvumilivu uwepo
Ester mmakasa
Me naonelea tusubiri mpaka ugonjwa uishe kabisa ili tuwe na uwakika kwenye michezo kwa usalama wa wachezaji wetu.
Zeiyana iddi
Korona imealibu mambo mengi
Sylvester
@Tim Meyer mechi zirudi hata kukiwa hamna mashabiki kuanzia kama June hivi
Daniel
If only we could get Champions League back soon
samiah
Corona imetuharibia kilakitu
Gabriel
Kwel hayo nimaamuzi sahihi
Neema juma
Jamanii corona imetutishia maisha