Loris Karius Awashtaki Besiktas na Kuomba Kukatishwa Mkataba

Mlinda lango wa klabu ya Liverpool, Loris Karius amevunja mkataba wake wa mkopo na Klabu ya Besiktas ya Uturuki, na mlinda lango huyo akitoa sababu kuwa ni kutolipwa mshahara tangu Januari… Karius amekuwa kwa mkopo huko Besiktas tangu 2018 na alikuwa anatakiwa kurejea katika Klabu yake ya Liverpool mwishoni mwa msimu.

Loris Karius

Mjerumani huyo alienda kuwashitaki Besiktas mwezi uliopita alipogonga mlango huko Shirikisho la Soka Duniani “FIFA” na kuomba ruhusa ya kuvunja mkataba wake na Klabu hiyo. Kipa huyo anadai kuwa hajapata kupokea mshahara wake kutoka kwa Besiktas tangu Januari na sasa amechukua hatua ya mwisho kukomesha mkataba wake na The Black Eagles.

Hakuna uthibitisho rasmi kutoka kwa Klabu, lakini kwa upande wake Karius Amethibitisha kuwa yeye sio mchezaji tena wa Besiktas…Anatarajiwa sasa kurudi Liverpool, ambapo bado yuko chini ya kandarasi nao, Liverpool ambao wamehusishwa na kutaka kumuuza msimu huu wa joto na klabu ya kwao Ujerumani, Werder Bremen ikimuhitaji..

11 Komentara

    nilijua ni bongo ndo wachezaji wanachelewa kulipwa mishahara kumbe hadi majuu pia, hii ndio faida ya kujiunga na meridianbet maana wanatupa habari motomoto

    Jibu

    Watu tunajuwa haya Mambo Ni Bongo tuu kumbe adi ulaya???!!!!!

    Jibu

    Moja wa golikipa mbovu wa liverpool. ..namkumbuka mechi ya fainal ya real madrid alichomesha.

    Jibu

    Dah bora apate team ya kucheza huyu jamaa na afute makosa yake…YNWA

    Jibu

    duuh kumbe janja janja sio bongo tu

    Jibu

    Harud nyumban aje kujipang upya kuanza moja so ujinga

    Jibu

    Jamani mpaka nje wanakuwa wababaifu kwa wafanyakazi wao.

    Jibu

    Me nikaju kwetu tu kumbe adi uko mambo aya yapo du

    Jibu

    Nilijuwa hapa kwetu tu ndiy kunashida ya
    Mshahar kumbe hata kwa wenzetu
    Kwel Hali Ni ngum

    Jibu

    Bora arudi

    Jibu

    Tunajuwa ni hapa bongo tu kumbe hata kwa wenzetu haya Mambo yapo duuuuh hatari

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.