Jurgen Klopp anasema ana furaha sana kutokana na ubora wa kikosi chake kwa sasa. Bosi huyo wa Liverpool inayokipiga kwenye Ligi Kuu ya Uingereza, Jurgen Klopp amesema kwamba bado anafurahishwa sana na kikosi chake cha kwanza cha klabu hiyo.
Katika madirisha matatu ya usajili ambayo yamepita klabu imetumia fedha kidogo sana katika usajili wa wachezaji wapya. Kwa sasa ni wazi kabisa kwamba Liverpool ndiyo klabu ambayo inapigiwa upatu kuja kuwa na utajiri mkubwa wa wachezaji.
Hata hivyo, ingawa wanaunganishwa kwenye dili za watu kama akina Jadon Sancho na Timo Werner, Klopp amesisitiza kuwa ametosheka sana na wachezaji ambao anao kwa sasa katika mikono yake klabuni pale.
Akiongea na beIN Sports, Mjerumani huyo anasema kuwa: “Sadio Mane ni kijana anyetosha kabisa na Mo Salah bado ni kijana muhimu kwetu na watakuwa hivyo kwa miaka kadhaa ijayo. Nina furaha sana kwa kweli, siwafikirii kabisa wengineo walio nje ya klabu.

“Nikiwa mazoezini na vijana wangu huwa sifikirii kabisa juu ya usajili wa wachezaji wengine. Kama tutasajili mbeleni tutaangalia uwezekano lakini kwa sasa tutatumia hawa hawa tulionao kikosini.”
Kwa sasa klabu yake ya soka ya Liverpool ina alama 25 zaidi ya yule anayefuatia kwenye msimamo wa ligi kuu ya Uingereza, Premier League.


Sylvester
Liverpool ni klabu bora kwa msimu huu na msimu ujao kama wachezaji maarufu wasipoondoka kama Sadio Mane,Firmino,Robertson,Van Dijik na Trent Arnold
mathayo sonje
sehemu unapopata mafanikio lazima ufurahie kama Klopp anavvofurahia kuwa Liverpool, maana ni timu yenye mafanikio makubwa kwa msimu huu.
Shafii
Klop ni kocha Bora Sana na kaweza kuendana na falsafa ya Liverpool ni jambo la furaha kwake
Ester mmakasa
Inafanya vizuri Liverpool hata mm nafurahia ilinapcheza.
Emnmy cleopa
Liverpool inafanya vzr sana napia huyo kocha jurgen klopp na namkubali sana
Ester mmakasa
Inafanya vizuri Liverpool hata mm naifurahia inapocheza uwanjani.
Ernest Kimeru
Klopp anastahili heshima kwa Mambo makubwa aliyoifanyia Liverpool kwa wakati huu.
Elika
Liverpool ni club Bora,huwa inajua nini inafanya poa hawajakosea hata lile neno la kwenye nembo yao,,,,I will never walk alone,safi sana kwa Liverpool chama la wana
Frank patrick
anahitajika kusajili hata wawili or amrudishe wilson na grujic aache kujiamini sanaa….YNWA
Lombo
liver wamekamilika haina haja ya usajili
Adelta
Liverpool Ni klabu nzuri Sana
Hawaitaji usajili
Njiku
Jurgen klopp ni bonge la kocha
Povel
Bonge la kocha kwa hv Sasa katika ulimwengu wa soka
Hopemwaikux
Kocha mzur sana huyu
Theckla
Klopp amejitoa Sana kuhakikisha Liverpool imefika mbali
Rehema Dickson
Ameisaidia sana Liverpool kufurahi ni haki yake
Ester jackson
Yuko vizuri sana