Waitalia Waliobamba Pale Premier League

Unadhani ni Di Canio? Zola? Ravanelli? Waliowika walipoichezea ligi kuu ya Uingereza?

Ni moja ya taifa ambalo limekuwa na vipaji lukuki na wachezaji bora sana waliotisha walipokuwa ama wawapo ndani ya ligi kuu ya EPL nchini Uingereza.

Wamekuwa na staili za aina yake na manjonjo makubwa sana wawapo uwanjani, hawa jamaa wameshinda FIFA World Cup mara nne na wameenda wakafanya vyema kule Uingereza.

Tangu kuanza kwa msimu wa soka wa mwaka 1992/93 kumekuwa na jumla ya wachezaji 76 waliowakilisha taifa la Italia kwenye Premier League, akiwemo Andrea Silenzi ambaye amekuwa ni wa kwanza alipoichezea klabu ya soka ya Nottingham Forest mwezi Agosti mwaka 1995.

Mojawapo ya mabao yaliyoweka historia ni yale ya akina Di Canio, Carbone, Zola, Pelle na wengineo wengi sana kutokea Italia.

 

Ubora wa Gianfranco Zola alipokuwa kwa klabu ya Chelsea alikuwa ni mchezaji muhimu sana kwa kufunga jumla ya magoli 59 na kusaidia upatikanaji wa mengine 42 kwa klabu hiyo.

 

Alikuwa na wenzake kutoka huko akiwemo Roberto Di Matteo pamoja na Gianluca Vialli, ambao wote hawa waliiwezesha klabu ya The Blues kushinda mataji kadha wa kadha huko Ulaya.

 

Ni Paolo Di Canio pekee ambaye amemzidi Zola ukiangalia kwa wale waliotokea Italia. Amefunga jumla ya mabao 66 na kusaidia mengine 49 akiwa na klabu za soka za Sheffield Wednesday, West Ham United na baadaye Charlton Athletic.

Takwimu zinazoongoza kutokea kwa wachezaji wa Italia waliocheza ndani ya PL

Mechi Magoli Assists
Gianfranco Zola 229 Paolo Di Canio 66 Paolo Di Canio 49
Paolo Di Canio 190 Gianfranco Zola 59 Gianfranco Zola 42
Benito Carbone 177 Benito Carbone 35 Benito Carbone 35
Carlo Cudicini 161 Fabrizio Ravanelli 25 Roberto Di Matteo 13
Alessandro Pistone 149 Graziano Pelle 23 Gianluca Vialli 11

 

Fabrizio Ravanelli aliwika ghafla akiwa katika klabu ya Middlesbrough msimu wa 1996/97, alifunga hatitriki katika wikiendi ya ufunguzi wa msimu akiwa na klabu yake dhidi ya Liverpool na kufunga jumla ya mabao 16, akawa sawa na Di Canio katika ubora kwenye msimu mmoja.

Kwa upande mwingine Benito Carbone alizichezea klabu tano tofauti ndani ya Premier League akiwa na klabu ya Sheffield Wednesday ambako alifanya vyema zaidi ya kokote alikokuwa.

Angalia takwimu bomba zaidi hapo juu kwenye jedwali na utuambie unadhani ni nani alifanya vyema akiwa Premier League alipotokea Italia?

  • Benito Carbone
  • Paolo Di Canio
  • Roberto Di Matteo
  • Fabrizio Ravanelli
  • Gianluca Vialli
  • Gianfranco Zola

13 Komentara

    Zola alikua bora sana kati ya hao kwa upande wangu.

    Jibu

    Di Canio hatari hapa ukiangalia records.

    Jibu

    Mim namkubali Sana zola

    Jibu

    meridianbet hamjawai mpo juu kwa habar moto moto

    Jibu

    Me nilikuwa namkubali sana Zola namba ya jersey yake ikastaafishwa kabisa pale chelsea

    Jibu

    Paolo di canio yupo poa

    Jibu

    Nilikuwah cjui Kama wababe wote wamekipgah sana nakukichafua vibaya sana Asante kwa habar Moto moto

    Jibu

    Axante kwa habar zenu nzur nzur

    Jibu

    Na ndo maana inaonekana kama ligi bora duniani kwa kuwa na wachezaji bora kutoka pande zote duniani.hao jamaa walikua ni hatari sana

    Jibu

    Good news 👍

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    Graziano Pelle , hajafanya maajabu makubwa sana ila napenda style yake ya uchezaji alikvyokuwa pale southampton

    Jibu

    inaonekana kama ligi bora duniani kwa kuwa na wachezaji bora kutoka pande zote duniani.hao jamaa walikua ni hatari sana

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.