Meneja wa Real Madrid, Zinedine Zidane anataka kutimiza ndoto yake ya kupata warithi wa nafasi tatu klabuni hapo. Zidane anataka kupata warithi wa Cristiano Ronaldo, Gareth Bale na Karim Benzema.
Katikia ndoto zake, Zidane anataka safu yake ya mashambulizi kuwa na Kylian Mbappe, Erling Halaand na Eden Hazard mpaka kufikia msimu wa joto wa 2021.
Wakuu wa Real Madrid wametajwa kuwa wanapania taratibu kumnasa Mbappe na Haaland, ikiwa ni ndoto ya Zidane kuwa na safu ya watatu hao baada ya kufanikiwa kumsajili Eden Hazard msimu wa joto uliopita.
Inakaaje hii? Mbape akiweka kambi kulia, Hazard akatia kambi kushoto, katikati tumshuhudie Haaland akidua hapo! Kwa mujibu wa chapisho la AS, Zidane anaamini itakuwa burudani sana kwenye mashambulizi.
Matumaini ya Zidane ni kuwa watatu hawa watakuwa na ladha ya watata watatu ambao ni Cristiano Ronaldo, Gareth Bale na Karim Benzema walivyokuwa wanaendesha mashambulizi.
Tangia kuondoka kwa Ronaldo, Real Madrid wanatajwa kuwa bado hawajapata ladha ile ile ya Ronaldo katika safu ya ushambuliaji. Itachukua mda kufanya hivyo. Ni matumaini ya Zidane kuwa watatu hawa watafaa zaidi kubadilisha utamu wa soka pale Real.
Hata hivyo kazi bado ipo kunasa sahihi za mastaa hawa! Wakati PSG wakiwa hawana mpango wa kumuachia Mbappe, Liverpool nao wamekuwa wakihusishwa naye. Man United wamekuwa wakihusishwa pia na Haaland. Real wakiweza kuruka viunzi hivi ndiyo wataweza kuboresha safu ya ushambuliaji ya ndoto za Zidane.


Lombo
mmmh si rahis
Hamidu
Itachukua muda kutengeneza timu yake.# meridianbettz
mwakalosi
Kwa kizazi hiki hakuna na hatawapata
Salma
Uwenda ikatimia ndoto yake
Antony Luseno
Kwa Ranaldo itachukua muda ila Bale na Benzema wanapatikana tu
Khadija
itachukua muda sana#meridianbettz
Frank Patrick
Mbappe asijiwahishe kwenda madrid tutamsahau …zidane awakuze wakina Assensio tu
Neema hassan
Asante kwa taarifa meridianbet
SADICK
Sio rahisi kupata chemistry anayotaka, mara chache hutokea kupata watu sahihi#meridianbettz
Gabriel
Pengo la Ronald bado mtihan
Mwajuma
Mm sizani kama ndoto itatimia maana cr 7 ni mtu mwingine
Povel
Thanks kwa meridian kwa information
Ernest
Huu mchukato mgumu sana nadhani wanahitaji muda kuwapata.
winfrida
anaweza kuwapata kwana wenyevipaji wako wengi na wanafanya vzr
Lydia Emmanuel Magoti
Atapatikana tuu
Warda
Zidane huwa hakosei
aisha
Itachukua muda sana
Theckla
mara chache hutokea kupata watu sahihi#meridianbettz
Isaya massawe
Itachukua muda kupata MTU kama CR7
Aziza mushi
Duh bado sana
Mwanaidi
Sio kirahisi kama wanavyofikiria
Evaluziga
Sio rahis wanavyofikilia
Ester jackson
Ni rahisi kama hao anaopambania wawe na nia ya kweli na kujituma kwa uhakika ndipo ndoto zake zitatimia
Samiah
Siyorahisi kumpata mtu km Cr7
Tahiya
Kupata kama wao na muunganiko wao sio rahis
David pere
Kuwapata Kama wale Tena ni kazi kubwa sana
Hope mwaikuka
Axante kwa taarifa
Carolyne
Good newz
Rehema Dickson
Mmh sio rahisi kama anavyo zani lakin ajaribu labda wanaweza tokea
Neema juma
Mmmh sidhani kama atafanikiwa
Furahav
Mmmh itskuwa hatar sana.
Genia skaluzwe
Ahsant kwa taarifa#meridianbeti
mathayo sonje
hii itakua vizuri japo ni kazi ngumu kwake
Emmy cleopa
Ahsante kwa taarifa
aisha
Ahsanteni kwa taarifa nzuri za kimichezo