Arsenal Kumbwaga Matteo Guendouzi Kwa Utovu wa Nidhamu

Nyota wa Arsenal Matteo Guendouzi hajafanya mazoezi na kikosi cha timu ya kwanza kwa zaidi ya wiki moja baada ya kupigwa marufuku na kocha wake Mikel Arteta. Mfaransa huyo amekuwa akifanya mazoezi binafsi pamoja na kocha wa viungo kwa kipindi cha wiki mbili zilizopita kufuatia vitendo vyake vya utovu wa nidhamu kwenye mchezo waliopoteza 2-1 dhidi ya Brighton.

Guendouzi alibahatika kutopata adhabu kwenye mchezo huo lakini kocha wake Mikel Arteta ameonyeshwa kukasirishwa na tabia ya kiungo huyo na ameamua kumtupa nje ya kikosi chacke. Alipoulizwa juu ya suala hilo, Arteta amesisitiza mara kwa mara kuwa tabia ya mchezaji huyo haijabadilika na bado Guendouzi ana shida ya utovu wa nidhamu.

Kwa mujibu wa Jarida la Athlete, Guendouzi aliitwa katika mahojiano na Arteta pamoja na mkurugenzi wa ufundi wa klabu Edu baada ya tukio la kumkaba Maupay wa Brighton na wawili hao hawakuridhika na majibu yake wakati alipoulizwa maswali juu ya tukio hilo.

Mfaransa huyo ameambiwa atakuwa akifanya mazoezi peke yake na mbali na wenzake hadi akijirekebisha tabia yake. Arsenal ilimsaini kiungo huyo mkabaji kwa pauni milioni 5 kutoka katika klabu ya Lorient na anatajwa kuwa mmoja wa wachezaji wenye nidhamu mbovu.

Kocha wa zamani wa Gunners, Unai Emery alikuwa akijua vyema matatizo ya utovu wa nidhamu wa Mfaransa huyo, ingawa alikuwa na imani angeweza kumbadilisha. Klabu sasa imepanga kukutana na wawakilishi wa Guendouzi katika siku zijazo kujadili mustakabali wake na inawezekana akaondoka klabuni hapo katika msimu huu wa joto.

Kwa sababu ya ukata wa kifedha wa Arsenal, klabu inaweza kupata pesa kwa mauzo ya kiungo huyo au kumtumia kama sehemu ya mabadilishano katika mkakati wake wa kumsaini kiungo wa Atletico Madrid Thomas Partey.

42 Komentara

    Bonge la makala

    Jibu

    Gud news

    Jibu

    Dogo unAjua nenda katafute changamoto nyingine #meridianbettz

    Jibu

    Pole yake.aache kukiuka sheria

    Jibu

    Duuuu kesha jiaribia sasa#Meridianbettz

    Jibu

    Gud news

    Jibu

    Asante kwa makala nzuri
    # meridianbet

    Jibu

    safi arteta hii itakua fundisho kwa wachezaji wengine apo klabuni

    Jibu

    Nichangamoto tu za mpila,we nenda kajaribu kwengine

    Jibu

    Mbona majanga kuwa moja wapo wa wenye nidhamu mbovu ila aombe samahani

    Jibu

    Dogo anajua ndiomaana kiburi kingi lakini hakisaidii km ivyo baada ya kuwa uwanjani wamemuweka benchi

    Jibu

    Sheria zimewekwa ili zifatwe sasa ujuaji wake katika mpira ndo afanye ivyo n makosa

    Jibu

    Yani hapo ulw usemi unaosema hakuna mxhezaji mkubwa kuliko timu Ndio inatimia Ndio maana wanammwaga

    Jibu

    Jeuri sio nzuri

    Jibu

    Utovu wa nidhamu sio nzuri unaweza ukajialibia

    Jibu

    Msameheni maisha mengine yaendelee kwa hakuna aliye kamilika

    Jibu

    Ujeri sehemu ya kazi siyo mzuri

    Jibu

    Guendouz ni mchezaji mzuri ila kwenye mpira unapokua huna nidhamu hata Kama ni fundi kiasi gani ni rahisi kipaji chako kupotea.

    Jibu

    Jeuri sio nzuri kwenye kazi

    Jibu

    Ujuaji mwingi na jeuri sehemu pa kazi havina maana siku zote mwisho wake hua mbaya ndio kama kinachompata hapo

    Jibu

    Bora aondoke

    Jibu

    Sheria ifatwe

    Jibu

    Makara manzuri

    Jibu

    duh!! ujeuri sio mzr jamani kashajiaribia#meridianbettz

    Jibu

    Kiburi chake kimemponza

    Jibu

    Nidhamu inahitajik

    Jibu

    Jeuli si uungwanaa

    Jibu

    Kwa sababu ya ukata wa kifedha wa Arsenal, klabu inaweza kupata pesa kwa mauzo ya kiungo huyo au kumtumia kama sehemu ya mabadilishano katika mkakati wake wa kumsaini kiungo wa Atletico Madrid Thomas Partey.# meridianbettz

    Jibu

    Hv nice update 👍

    Jibu

    Hutovu wa nidham co kitu kizuli so wamteme tu na co kumwaga pekeyake

    Jibu

    Makala imeeleweka

    Jibu

    Nimaamuz ya harak wampe tena nafax

    Jibu

    asante kwa makala

    Jibu

    Kocha amefanya vizuri iwe fundisho kwa wengine..

    Jibu

    Acha tuu arteta amfundishe adabu maana anabidi awe na nidhamu

    Jibu

    Pole yake

    Jibu

    Safi sana Arteta, hii nzuri sana atajifunza siku nnyingine

    Jibu

    Maoni:Kweli Arteta mwalimu!

    Jibu

    Viwango vya wachezaji vinapotea kwa kukosa nidhamu.

    Jibu

    Hakuna mchezaji mkubwa kuliko team Arteta akiendelea hvyo atakuja kupata mafanikio sana kwenye kipindi chake cha ukufunzi

    Jibu

    Utovu wa nidhamu co mzuri awe mfano kwa wengne

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.