Bwalya na Hadithi ya Vibanda Vitatu

Kwanza wacha niihusie nafsi yangu kabla sijahusia nafsi ya mwingine kwenye yale yote mema ikiwemo kumtamkia mema binadamu mwenzako, naombeni Kumbukumbu la Torati kwa kalamu yangu nilipigia mstari maneno matakafitu

Rejea Marko 9:5 inasema “Mwalimu, ni vizuri sisi kuwapo hapa, Basi, afadhali tujenge vibanda vitatu, Kimoja chako, kimoja cha Mose na kimoja cha Elia”, nilipenda sana kusikia hadithi hii juu ya ujenzi wa vibanda pale Mlimani, nami nataka nimsafirishe Bwalya mpaka nyuma ya muda kumpa historia ya vibanda vitatu

Najua nimeanza na gubu sana, sijakukaribisha Tanzania najua nimevunja sheria zetu za ujamaa aliotuachia Mwalimu Nyerere, pengine imetokana na haraka zangu nyingi kutaka kumaliza hadithi yangu kwako, najua miguu ni ya dhahabu na akili ya computer, najua hilo

Naomba tupande kwenye milima ya Uluguru Morogoro mji kasoro bahari, kibanda cha kwanza wala sio cha Elia, kumbuka tumerudi kwenye maisha ya kawaida, kibanda hiki aliishi Patrick Mutesa Mafisango, usisahau

Moja Kati ya Viungo bora kutokea nchini, ile juu ni jezi yake namba 32, vile chini ni viatu vyake vya Adidas, pale pembeni ni maua na mashada ya mashabiki wa Simba, waliohusudu soka lake kuliko chochote

Kibanda hiki cha Mafisango hakina mtu kwasasa, kama uonavyo Mjumbe wa Mtaa mlangoni, mwenye kibanda chake ametangulia mbele za haki, ila ndani kuna vitabu na Kila kitu kwa ajili yako kurithi

Ikiwapendeza Simba watakupa funguo ufungue, ukutane na bidii, kipaji na roho Ngumu, ikiwapendeza lakini, wao wenyewe wenye Simba yao sio Mimi, uyakutayo ni wewe kuamua sasa

Rally naomba tupite kwenye kibanda hicho tusogee kwenye kibanda cha Pili, nadhani umekiona kilivyojitenga, hapa anaishi Mtoto wa Msimbazi, kipenzi chao aliefika hapa akiwa na miaka 19 tu, hakutumia pesa kuishinda mioyo yao, bali miguu yake kwenye viwanja vya Vita

Alitokwa jasho hata kama mvua inanyesha, angepiga kelele kuwaamsha wenzake, kuna muda aliamua mechi kupitia miguu yake, anaitwa Emmanuel Okwi The Prince of Simba, najua unashangaa taa inawaka na walinzi wapo nje wanalinda hatuwezi kuingia ndani kumradhi

Itaendelea..


FURAHIA KASINO YA MTANDAONI

Tembelea ardhi ya maajabu ushangazwe na mengi ikiwa ni pamoja na urahisi wa kujipatia utajiri kupitia Kasino ya Meridianbet.

Cheza Sasa

27 Komentara

    kumbukumbu nzuri

    Jibu

    Gud

    Jibu

    Kweli hi ni hadithi ya vibanda vitatu.na inahusiana kabisa

    Jibu

    Mashujaa hao watazidi kukumbukwa na ndio walio hifanya simba hionekane Leo hii r i p okwi
    r i p mafisango

    Jibu

    Vizuri Sana Bwalya

    Jibu

    Good 👍

    Jibu

    Gud news.

    Jibu

    Hadithi ya vibanda vitatu inasisimua ajabu ahsanteni sana

    Jibu

    Good news

    Jibu

    Kweli hadithi ya vibanda vitatu ila mashujaa hao watazidi kukumbukwa

    Jibu

    Hadithi nzuri inatuelisha na kutufundisha

    Jibu

    Bwalya simba ni kama hawataelew kabumbu lako ila mida itaongea

    Jibu

    Nmetoka kapa

    Jibu

    Safi sana

    Jibu

    Mashujaa hao watazidi kukumbukwa

    Jibu

    Safii

    Jibu

    Fresh

    Jibu

    Makala nzuri mwandishi umeweza kututeka hisia zetu kwenye kusoma neno moja adi lingine, Kazi nzuri sana

    Jibu

    Mafisango ni kiungo wa level nyingine kabisa ambae hawezi kusahaulika ndani msimbazi#meridianbettz

    Jibu

    Mtu hatari sana huyu pale msimbaz

    Jibu

    Kweli hadithi ya vibanda vitatu ila mashujaa hao watazidi kukumbukwa

    Jibu

    Wakumbukwe daima

    Jibu

    Akumbukwe alivyokua shujaa

    Jibu

    imekaa vizuri sana hii hadithi

    Jibu

    Ni mashujaa wa nchi kumbu kumbu zao zimeandikwana haziwezi kusahaulika kabisa

    Jibu

    Bwalya mtu sahihi pale Msimbazi

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.