Ozil Alivyonikumbusha Stori ya Vieirra

Arsenal wameenda vyumbani kupumzika, kipindi cha kwanza kilikuwa kigumu haswa. Fulham wamekuwa wakorofi, wamewadhibiti Arsenal vilivyo. Arsenal wanatembelea ‘mtungi’, pumzi imewakatikia, wanasubiri tu kurejea ili wakafungwe. Si kwa moto waliowashiwa kipindi cha kwanza na Fulham.

Wachezaji wote wakiwa wamekaa chini wanasubiri maelezo ya Arsene Wenger aliingia Patrice Vierra, moja kwa moja akamfuata Nikolas Anelka akamuambia “Tungeweza kutoka tunaongoza, ila kwa ujinga wako umekosa nafasi ambayo hata mwanangu wa miaka mitano angepata. Halafu haukabi kabisa, unazurura tu uwanjani. Kama unapenda kutembea sana usingekuja Arsenal, ungeenda kuwa muigizaji wa ufukweni na mkeo”.

Nikolas Anelka akavimba, akamuambia Vieirra “Wewe unanikaripia kama nani? Hicho kitambaa tu cha unahodha ndio kinakupa kiburi? Kama unadhani ni rahisi, njoo wewe ucheze namba tisa”. Hapo ndipo Vieirra akavaa ule ukichaa wake halisi. Akashusha bukta yake akabaki uchi kisha akamuambia “Mimi ni nahodha hapa lakini kabla ya unahodha mimi ni mwanaume. Shusha macho yako unitazame vizuri. Ndiyo maana nafanya kazi za kiume pale katikati ya uwanja. Sirembui kama wewe. Acha upumbavu, turudi tukaipiganie Arsenal. Mimi na wewe ni mali ya hii klabu.”

Arsene Wenger alimuita Vieira pembeni akampa tano akimpongeza kwa nzuri ya unahodha anayofanya. Licha ya yeye kuwa kocha, hakuwa na uwezo wa kufoka kama Vieirra. Robert Pires anasema ilifika kipindi wakawa wanamuita Vierra Tyson , hakuna mchezaji aliyekuwa na uwezo wa kukohoa mbele yake. Akisema kimya kila mchezaji anafunga mdomo.

Nimekikumbuka hiki kisa baada ya kuiona picha ya Mesut Ozil akiwa na kitambaa cha unahodha. Hivi ni kweli Ozil huyuhuyu amewahi kuwa captain wa timu?

Nimekumbuka pia Patrice Vierra alivoondoka Arsenal. Aliona imani ya kocha kwake imepungua. Isitoshe Cesc Fabregas alishaandaliwa vema kumrithi. Akaona hana cha kusubiri, japo ilikuwa ngumu, akafanya maamuzi akaondoka. Nimekumbuka alivoondoka Patrick Vieira baada ya kutokumuona Ozil kwenye kikosi cha kwanza. Hata benchi siku hizi hayupo, vijana wameaminiwa zaidi. Anasubiri nini zaidi?


FURAHIA KASINO YA MTANDAONI

Tembelea ardhi ya maajabu ushangazwe na mengi ikiwa ni pamoja na urahisi wa kujipatia utajiri kupitia Kasino ya Meridianbet.

Cheza Sasa

30 Komentara

    makala nzuri

    Jibu

    Asantee kwa makala

    Jibu

    Dah jmn hichi kisa ni atari.kavua nguo uwanjani

    Jibu

    Arsenal ya Wenger ndio ilikua ya moto sasa hivi akuna kitu

    Jibu

    Arsenal ilikuwa kipindi hicho asaivi Amna timu humo

    Jibu

    Ozil kama ni mpira kashacheza sana bora arudi nyumbani ujerumani astaafie kwao

    Jibu

    Makala nzuri Sana

    Jibu

    Makala imesimama sana patrick viera alikua kiungo matata Sana.

    Jibu

    Arsenal ilikua zamani sasa ivi haina maajabu kabisa

    Jibu

    Good news

    Jibu

    Asante kwa nakala

    Jibu

    Patrick Viera ilikuwa shughuli nyingine pale ktkt ya uwanja na ndivyo Nahodha unatakiwa kuwa hivyo#meridianbettz

    Jibu

    Arsenal ya zaman ndio ilikua mpango mzima lakn asaivi hamna kitu

    Jibu

    Kipindi cha nyuma arsenal ilikuwa moto

    Jibu

    Makala nzuri

    Jibu

    Ozil asepe the gunners hana chake

    Jibu

    Uamuz upo kwake

    Jibu

    Maamuzi yapo kwake

    Jibu

    Ozil kama ni mpira kashacheza sana

    Jibu

    Ozil kiwango kimeisha

    Jibu

    Maamuzi yake

    Jibu

    Tunaweza sema Arsenal watakuwa vizuri sana kipindi hiki lakini Binafsi siwaoni Arsenal kama timu tishio ndani ya EPL

    Jibu

    The gunners mtu kama ozil unamwekaj nje ndio maana wanafeli kweny ubingwa

    Jibu

    Tunaweza sema Arsenal watakuwa vizuri sana kipindi hiki lakini Binafsi siwaoni Arsenal kama timu tishio ndani ya EPL

    Jibu

    Vierra kama vierra jembeee

    Jibu

    Vierra mtu mbaya

    Jibu

    wenger alikuwa anajua jinsi ya kuwatumia vizuri wachezaji wake

    Jibu

    Patrick alikuwa mchezaji matata sana

    Jibu

    Arsenal ni gari la mkaa muda wwte linazima lile

    Jibu

    Habari nzuri.

    Jibu

Acha ujumbe