Wakati michezo ya ligi mbalimbali ikirudi wikiendi hii. PSG wanamashaka na kikosi chao kufuati idadi ya majeruhi kuongezeka.
PSG watakuwa uwanjani kesho (Ijumaa) kupambana na Nimes katika muendelezo wa Ligue 1 kabla ya kuwakaribisha Man United mapema Jumanne wiki ijayo ikiwa ni mchezo wa kwanza wa UEFA msimu huu.
Thomas Tuchel anapata kigugumizi kwa idadi ya wachezaji ambao anadhani wapo tayari kuipeperusha bendera ya Paris Saint Garmain katika michezo hiyo. Mpaka sasa, majeruhi, mechi za kimataifa na utaratibu mpya wa kujilinda na COVID19.Ni vikwazo kwa Tuchel.
Akizungumza na vyombo vya habari kuelekea mchezo wa kesho, kocha wa PSG – Thomas Tuchel amesema, “Draxler, Verratti na Marquinhos hawatocheza dhidi ya Nimes na pia ninamashaka juu ya uwepo wao kwenye mchezo dhidi ya Man United.
“Herrera alipata COVID19. Danillo alikuwa na Cristiano Ronaldo hivyo hawezi kujiunga na sisi kwa sasa.
“Kehrer bado ni majeruhi na ataendelea kuwa nje kwa wiki chache zijazo.Bernat pia hayupo na sasa Icardi pia aliumia kwenye mazoezi na hatokuepo kwenye mchezo dhidi ya Nimes na Man United.
“Tunahitaji kikosi cha wachezaji wenye kujiamini zaidi. Katika mchezo wa kesho, tunataka kushambulia zaidi na kuzuia kufungwa magoli mengi. Tunatakiwa kuwa tayari kwa ajili ya Manchester United.
“Kwa upande mwingine, tunatakiwa kuwamakini na wachezaji waliorejea kutoka kwenye michezo ya kimataifa kama Mbappe na Neymar. Labda tutakuwa na wachezaji 11,12 au 13.”
Naam, hapa ni mahali pako! Kuwa shujaa kwenye sloti hii ya Samurai Ken ujishindie mkwanja na kujipa burudani murua.



felister
kikubwa ni kujituma na kufanya mazoezi zaidi kwa kufanya ivyo mtafanya vizuri psg
David Pere
Ni mtihani mkubwa Sana kwao maana haielewski Kama itawezekana au laa
Janeflora malisa
Vzr wajipange kwa bidii
Mwanahamisi
Kikubwa ni kuongeza juhudi
zeiyana
psg wanawakati mgumu sana
Adelta
Naona wafanye juhudi na kuimarisha upya vikosi
Tahiya
Never give up
Caroline
P.S G poleni sana.mna majeruhi wengi sijui itakuaje gemu inayofatia
magdalena
hakuna kukata tamaa kikubwa kupambana na kusonga mbele zaidi bila kuangalia nyuma
Sauda
Mazoezi muhimu
Saupha mohamed
Muhimu kupambambana
Mwajumah
Psg wanawakati mgumu sana
Fatina mfigi
Kikubwa kupamban tu wasikate tamaa matokeo yatakuwa mazur
Lydia Emmanuel Magoti
PSG game nawaona inawapa changamoto za kutafakali itakuwaje Kama kuiletea huoga
Antony Luseno
Nice update #meridianbettz
Ernest
Kweli ni changamoto kubwa kwa PSG kutokana na list la wagonjwa lakini hawana budi kupambana bado wana kikosi kipana
Tatu
Psg wana wachezaji wakubwa wazuri tu ila awajiani bado
Dorophina
Psg wanamtihani mkubwa sana cha msingi wasikate tamaa
Hopemwaikuka
PSG wajipange sana
Gabriel
Kikubwa kupamban t
Povel
Changamoto kubwa sana inabid wapambane tu hapo
Sabrina
Wakaze tu
Issa
Psg inabid watafute mbinu mbadala
aisha
Psg wakaze kweli kweli
Chiku
Wasikate tamaa