Tetesi zinasema Chelsea imejiunga katika kinyang’anyiro cha kumsajili mshambuliaji wa Borussia Dortmund Erling Braut Haaland, 20.
Matumaini ya Manchester United katika kumsajili Halaand huenda yakadhoofishwa kutokana na uhusiano wake na wakala Mino Raiola, ikimaanisha kwamba mshambuliji wa Everton Dominic Calvert-Lewin, 23, huenda akawa mbadala wa kikosi cha Ole Gunnar Solskjaer.
Tetesi zinasema Paris St-Germain inamnyatia Rudiger, huku beki huyo akipata tatizo la kujiunga na kikosi cha kwanza katika klabu ya Stamford Bridge.

Liverpool ina hamu ya kumsajili beki wa Real Madrid na Eder Militao, 22, huku mchezaji huru wa Argentina Ezequiel Garay, 34, akitarajiwa kujiunga na klabu ya Jurgen Klopp.
Mikael Arteta na Arsenal wanataka kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid na Brazil Vinicius Jr, 20, kwa mkopo mwezi Januari , lakini wameamua kumsajili mchezaji mwenza na kiungo wa kati wa Uhispania Isco, 28, ambaye anatarajiwa kujiunga na Juventus.
Tetesi zinasema Barcelona imeanza mazungumzo na beki wa Arsenal na Ujerumani Shkodran Mustafi, 28, ya uhamisho wa bila malipo wakati kandarasi yake itakapokamilika mwisho wa msimu.
Mkufunzi wa klabu ya Derby county Wayne Rooney anataka kumsajili mchezaji wa Man United na England Phil Jones, 28, kuwa mchezaji wake wa kwanza kumsajili katika timu hiyo ijapokua Rams huenda ikakabiliwa na ushindani kutoka kwa West Brom na Burnley.
Tetesi zinasema Everton na Wolves wanatarajiwa kukabiliana na AC Milan katika kumsajili beki wa Strasbourg na Ufaransa Mohamed Simakan, 20, ambaye anapatikana kwa dau la £20 million.

Kipa Loris Karius, 27, huenda akarudi katika klabu yake ya Liverpool, baada ya Union Berlin kufikiria kusitisha kandarasi yake mapema huku mchezaji hyo wa Ujerumani akichezeshwa mara moja tangu kuanza kwa msimu.
Barcelona inajaribu kumsajili kiungo wa kati wa Uhispania Ruqui Puig kutia saini kandarsi mpya , lakini Manchester City na Bayern Munich zote zinamtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21.
VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!
Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini???



Ernest Kimeru
Loris Karius anatakiwa aachane na Soka kabisa
farida ahmad
Asante kwa taarifa
Saupha mohamed
Good news
Adelta
Afanye mambo mengine
Shakila mrope
Asante kwa taarifa meridian bert
Rahmal
Shukrani kwa taalifa
Caroline
Asante kwa taarifa
Mwanahamisi
Gud news
Lydia Emmanuel Magoti
Habari nzuri
Issa
Imekaa poa
Hopemwaikuka
Haalad akienda man u ndo poa
Tatu
Habari nzuri
Sarah
Iko poa
Angelina
Goodupdstte
warda
Man U kila wakikaribia kupata mchezaji mzuri inatokea vikwazo
Chiku
Kila penye zuri baya lipo