Mashindao ya kimataifa kwa wachezaji wa ndani – Chan 2021, yameanza kutimua vumbi nchini Cameroon. Tanzania imeanza kwa kipigo dhidi ya Zambia.
Taifa Stars wameshindwa kuitumia vizuri karata ya kwanza kwenye mashindano ya mwaka huu baada ya kuruhusu kufungwa 2-0 katika mchezo wa kwanza dhidi ya wanachipolopolo.
Mchezo ulianza kwa timu zote kutokuwa na utulivu zikishindwa kutambua ni kipi hasa zinatafuta. Kipindi cha pili mambo yalibadilika, Stars walianza kutafuta nafasi za kufunga lakini Chipolopolo walizitafuta na kuzitumia vyema nafasi zao.
Shomari Kapombe aliushika mpira katika eneo hatari na kuwazawadia Zambia mkwaju wa penati kunako dakika ya 62. Sikombe aliitumia vyema nafasi hiyo na kuwapatia Zambia goli kupitia mkwaju wa penati.

Almanusura Sikombe apachike goli la pili katika dakika ya 75 lakini umahiri wa Aishi Manula uliwaokoa Stars baada ya kumzidi ufundi Sikombe ambaye alibaki yeye na kipa huyo.
Dakika ya 82, Zambia walimaliza mchezo baada ya Sikombe kutoa pasi maridadi kwa Chabula ambaye alipachika goli la 2 na kuwapatia Chipolopolo pointi 3 muhimu katika mchezo wa kwanza wa mashindano ya Chan 2021.
Stars sasa wanahitaji matokeo ya ushindi katika michezo miwili iliyosalia kwenye hatua ya makundi. Mchezo unaofuata, Stars watachuana na Namibia kabla ya kucheza na Guinea katika mchezo wa mwisho wa hatua za makundi.
Pokea mualiko wa Meridianbet na Pragmatic Play kutengeneza mkwanja kwenye kasino ya mtandaoni sasa. Jiunge sasa kupata ishindi huu.



Adelta
Tusikate tamaa tujipange kwa mechi zinazokuja
Sadick
Zambia ni timu nzuri na inauzoefu wa mashindano haya. Ni imani yangu tutashinda dhidi ya Namibia na Guinea
Mwanahamisi
Asante kwa taarifa
Venerose
Tuongeze bidii tutashinda
Magdalena
Tanzania inabidi ijipange vyema kwa ajili ya michezo ijayo
Angelina
Naamini bado wana nafasi yakufanya vizuri
Dorophina
Tanzania wamekutana na timu nzuri ndiomaana ikapigwa
Rahmal
Abali njema
Lydia Emmanuel Magoti
Kawaida ndio mchezo huo
Hopemwaikuka
Pole yao
Sarah
Ndio mchezo ulivyo
felister
tuongeze bidii tutafanikiwa
Neema juma
Sio mwisho wa mchezo wasikate tamaa
Ester mmakasa
Taifa stars jamani wamejuwa kutuumbua mashabiki wao.
Janeflora malisa
Asnt kwa taarif meridianbet
Shakila mrope
Ndo mchezo huwo
Sabrina
Taifa 🌟 wanatakiwa wakaze
Ernest Kimeru
Tanzania katika Soka ni kichwa cha Mwendawazimu
Mwanahamisi
Ndio mchezo ulivyo
warda
Watasonga tu