Mchezaji mshambuliaji wa Tanzania na KRC Genk, Mbwana Ally Samatta yupo katika majadiliano na Levante ya huko Ligi Kuu ya Hispania ili kuona namna wanavyoweza kukamilisha mpango wa yeye kuhamia klabuni kwao.
Dau lake
Klabu ya Levante imetenga kitita cha Euro milioni 4 ili kumsajili Samatta ingawa klabu anayoitumikia kwa sasa imegomea ofa hiyo na kuhitaji euro milioni 8 ili wamuachie.
Endapo ataweza kutimkia huko Levante ni dhahiri kuwa atacheza Ligi moja na mwamba wa soka wa dunia, Lionel Messi wa Barcelona ambapo wakala wa Samatta amethibitisha kuwepo kwa mazungumzo baina ya klabu hizo mbili huku miamba ya Urusi ambao ni CSKA Moscow wanamhitaji sana pia.


Devotha
🔥🔥
Lydia Emmanuel Magoti
Habari njema kwa mchezaji huyo samatta
Nasra
Samatta anatupa raha mashabiki zake