Usajili: Mourinho Anataka Beki wa Kati Mkali!

Jose Mourinho anatakiwa kumpiga bei beki mmoja wa kati ili asajili wakali wengine kwenye timu yake ya Manchester United inayoshiriki Ligi Kuu ya Uingereza.

Amesema kuwa anataka msimu ujao awe na kikosi imara ili ahakikishe klabu hiyo inanyanyua Kombe la Ubingwa wa Uingereza EPL ambao waliukosa msimu uliopita wa mwaka 2017/18.

Anayemlenga

Kwa sasa Mourinho anatakiwa kumpiga bei beki mmoja ili apate saini ya beki Harry Maguire kutoka Leicester City na pia anataka kuhakikisha kwamba kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili anampata beki wa AC Milan, Leonardo Bonucci.

Pia, anataka kumsajili Toby Alderweireld wa Tottenham Hotspur ikiwa na maana kwamba atatakiwa kumpiga bei beki wake Chris Smalling klabuni hapo.

3 Komentara

    Mourihno hanaipenda sana man Chester ukiondoa beki pia nishabiki wa man..!tujiandae kupokea ushindi tu mashabiki

    Jibu

    Duuh kazi

    Jibu

    Habar njema

    Jibu

Acha ujumbe