Kipa Marcus Bettinelli ameripotiwa kukubali kutia saini mkataba wa miaka miwili na klabu ya Chelsea.
The Blues wamekuwa sokoni kusaka golikipa wa chaguo la tatu baada ya mkongwe Willy Caballero kuondoka kwa uhamisho wa bure mwezi uliopita.
Kipa wa zamani cha Crystal Palace Wayne Hennessey aliaminika kuwa mlengwa wa Chelsea kabla ya kuamua kusaini mkataba na Burnley.

Kwa mujibu wa Daily Mail, Chelsea sasa iko katika hatua za mwisho za makubaliano na Bettinelli, ambaye alikuwepo Fulham.
Alitokea katika Akademi ya soka ya West Ham, na sasa akiwa kijana wa miaka 29 aliweza kucheza jumla ya mechi 120 za mashindano yote kabla ya kuondoka mwishoni mwa mwezi Juni.
Bettinelli alitumia msimu uliopita kwa mkopo huko Middlesbrough, akicheza mechi 41 kwenye Mashindano.
SHOOT! mchezo unaokupa nafasi ya kupambania ushindi wako mkubwa kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet! Usisubiri hii, jiunge sasa kufurahia ushindi!



Sarah
Vizuri
Angelina
Good