Mkufunzi wa timu ya Rivers United Stanley Eguma,amewahakikishia mashabiki wake kuwa hawataruhusu hata goli moja kutoka kwa timu ya Yanga, watakayocheza nayo katika mechi ya marudiano itakayopigwa nchini Nigeria septemba 19 siku ya jumapili.
Rivers United wanafaida ya ushindi walioupata nchini Tanzania wa goli 1-0 huku wakitoa malalamiko lukuki kwa wenyeji wao katika mechi hiyo.

Rivers united imepanga kuwafungulia mashtaka klabu ya Yanga dhidi ya mashabulizi yaliofanywa na mashabiki wao siku ya mechi. Chris Green alisema “tutawafungukia mashitaka kwa vitendo vyao visivyo vya kiungwana ili iwe fundisho kwa wengine.”
Pia aliongezea “tulifanya vipimo vya Uviko-19 Nigeria na kukutwa hatuna maambukizi, “lakini tulipofika Tanzania saa tatu kabla ya mechi kuanza tulishangazwa kuwa tunahitajika tena kupima.”
“Tulipofika uwanjani bado walitaka kuwa na uhuru wa sehemu yetu ya kubadilishia nguo, “nje walimpiga mwanahabari wetu, “baada ya mechi kuisha walituondolea gari ya kutusindikiza kurudi hotelini.”
Tutafungua mashitaka CAF kupitia NFF, ushaidi wote tunao, sisi tutawapokea vizuri na kuwatendea vizuri.
Unaanzaje siku yako na kuimaliza bila kupitia katika kasino bomba za meridianbettz, mchezo mashuhuri wa Disco Funk unaweza kukufanya uwe mshindi leo hii.!


