Kocha wa Al Ahly Sc 🇪🇬 Pitso Mosimane alivyomjibu kwa hasira mwandishi wa habari baada ya kuhoji uwezo wa winga wa timu hiyo Luis Miquissone ambaye bado hajaonyesha makali yake tangu ajiunge na timu hiyo
“Kwahiyo unataka Luis asicheze, Kwanini asicheze, mbona wachezaji wengine hujauliza, kwanini Luis”

“Ni nani aliyesababisha faulo ya ushindi, tumepata goli kutokana na kazi ya nani?”
“Luis ni mchezaji wa Al Ahly na atacheza hapa, atapata nafasi kama Hamdy na atapata nafasi kama wachezaji wengine, kila mmoja ni mchezaji wa Al Ahly, hapa atacheza”
“Nitamtoa Tau, nitamtoa Sherif na nitamtoa hata Afsha, hapa hakuna star, wachezaji wote ni sawa”
Al Ahly Sc 🇪🇬 hapo jana waliibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Ghazl El Mahalla huku goli la ushindi likipatikana dakika ya mwisho ya mchezo
Wiki nyingine ya kushinda mamilioni ukiwa na kasino maridhawa za meridianbettz. Mchezo pendwa wa Fai Cai Shen unakupa thamani ya dau lako, kwa kiasi kidogo cha dau unaweza kushinda mkwanja mrefu.


