Klabu ya Paris Saint-Germain inaripotiwa kuwa wanatarajia kumalizana na wachezaji takribani saba katika dirisha la uhamisho la mwezi Januari.
Les Parisiens wameanza vyema msimu wa Ligue 1, wakiongoza jedwali la ligi kwa pointi 11, pia wakifuzu hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa.
Wachezaji wanatarajiwa kuingia Januari ni wachache sana kwa PSG, lakini kwa mujibu wa L’Equipe, klabu hiyo inatarajia kuwahamisha wachezaji kadhaa ambao wamepoteza mvuto kwenye kikosi cha PSG kwenye dirisha la majira ya baridi.

Ripoti hiyo inadai kuwa Sergio Rico, Rafinha, Eric Ebimbe na Layvin Kurzawa watakuwa wa kwanza kusepa klabuni hapo.
Zaidi ya hao, Colin Dagba na Abdou Diallo wanadaiwa wamekuwa ni ziada kwa mahitaji ya Mauricio Pochettino, wakati Mauro Icardi pia yuko kwenye mpango wa watakaosepa.
PSG wanadaiwa kutaka karibu €50m (£42.7m) walizolipa awali kwa Icardi ili kuidhinisha biasahara hiyo, ingawa hakuna mchezaji hata mmoja kati ya hao saba anayetarajiwa kuwa mchezaji huru mwakani 2022.
Unaweza kujishindia mamilioni katika kasino yako pendwa ya meridianbettz, mchezo wa Agent Jane Blonde Return ni moja ya michezo inayopendwa kwasasa huku ikiwafanya wachezaji kuwa mamilionea kila siku. Unasubiri nini! ungana na Agent Jane Blonde akufanye milionea.
CHEZA HAPA


