Tetesi zinasema, Newcastle inakabiliwa na ushindani kutoka Manchester United na Tottenham katika kinyang’anyiro cha kusaini mkataba na mlinzi wa England Kieran Trippier, 31, kutoka klabu ya Atletico Madrid.
Tetesi zinasema, Tottenham, Newcastle, West Ham na Rangers wanagombania kusaini mkataba na mlinzi wa West Brom na England Sam Johnstone, 28.
Tetesi zinasema, Arsenal wako tayari kusikiliza ofa kwa ajili ya mshambuliaji wa Gabon Pierre-Emerick Aubameyang, 32, baada ya kuvuliwa unahodha mwezi huu.

Napoli wanaangalia uwezekano wa kusaini mkataba na beki wa Everton na Ufaransa Lucas Digne, 28, ambaye amedokeza kuwa anataka kuondoka katika Goodison Park mwezi Januari.
Liverpool wanamfuatilia kwa karibu winga wa Porto na Colombia Luis Diaz, 24, kama mchezaji mbadala wa Sadio Mane, 30, ambaye anaelekea kwenye michuano ya Kombe la mataifa ya Afrika ambapo atailichezea taifa lake la Senegal mwezi ujao.
Mshambuliaji wa Canada Jonathan David, 21, ambaye amekuwa akihusishwa na Arsenal na West Ham, ataondoka katika klabu ya Lille ya Ufaransa mwaka ujao, amesema wakala wake.
Barcelona wako tayari kupokea kofa kwa ajili ya mlinzi wa Marekani mwenye umri wa miaka 21 Sergino Dest, huku Bayern Munich nao wakifuatilia hali yake ya kimchezo.

Tetesi zinasema, Newcastle wamejiunga na Brighton katika mbio za kusajili mlinzi wa Tottenham na Wales Joe Rodon, 24.
Borussia Dortmund watajaribu kusaini mkataba na kaka yake Jude Bellingham, Jobe, 16, ili kumshawishi kiungo wa kati wa England, 18, kuendelea kubaki Signal Iduna Park.
Nani hapendi kuwa bingwa na kujishindia mkwanja wa kusahato kuelekea katika sikukuu wiki hii. Mchezo wa Ocean Call kutoka kasino maridhawa za meridianbettz unakupa kila sababu ya kuifanya siku kuu yako kuwa ya kuvutia zaidi.


