Bingwa ligi ya Ufaransa Ligue 1 PSG wanaamini wanaweza kumshawishi nyota wao ambae mkataba wake unakwenda kuisha majira ya kiangazi kuweza kusalia kwenye klabu hiyo kwa angalau miaka miwili zaidi.
Mpaka sasa klabu ya PSG wamegoma kukubali kuwa mchezaji huyo anaweza kuondoka licha kuzuka taarifa ya kuwa Mbappe anavutiwa zaidi na klabu ya Real Madrid na anahitaji kwenda kujiunga na klabu hiyo.
Huku mama wa mchezaji huyo akithibitisha kuwa hakuna makubaliano yoyote yaliofanyika na klabu ya PSG, wala na klabu nyingine yoyote mpaka sasa, mpaka sasa Mbappe anaweza kufanya makubaliano na klabu yoyote kwa utulivu kabisa na kufanya uchaguzi sahihi .
Inaaminika kabisa kuwa huu mwezi hautakwisha bila ya hatma ya mchezaji huyo kujulikana, ikiwa atasalia kwenye klabu hiyo au atajiunga na klabu ya Real Madrid au klabu nyingine yoyote.
Mshindi huyo wa kombe la dunia mkataba wake na miamba hiyo ya Ufaransa unakwisha bdmwishoni mwa msimu na Real Madrid ndui timu pekee inayoonesha nia ya kuhitaji huduma ya mchezaji huyo mwenye miaka 23.
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.