Vuta Nikuvute ya Chama Kubaki Simba au Kwenda Yanga

Katika pita pita zangu mtandaoni nikakuta post yenye picha ya Clatous Chama iliyopostiwa na Deo mwanasoka ikigusia taarifa za wanasoka nguli duniani na ambavyo pesa imeweza kubadiri matakwa ya mioyo yao na kwenda pesa ilipo.

Clatous Chama
Clatous Chama

Kwenye post hiyo kunaonenasha dhahir kua lile linaoendelea mtandaoni kumuhusisha Clatous Chama kujiunga na Mahasimu wakubwa wa timu ya Simba Sports Club yenye makao yake makuu eneo la msimbazi jijini Dar es Salaam, ingawa taarifa hizo za Clatous Chama kujiunga na klabu ya Yanga Africa bado hazijarasimishwa,

Kwanini Tunafananisha Tukio la Chama na Yaliyopita

2013 Brazil wakiwa bize kuandaa kombe la dunia, kocha Luis Felipe Scholari aliulizwa anafikiria kumuita nani akaongoze safu yake ya ushambuliaji sambamba na Neymar Jr? Scholari alijibu kwa madaha na kebehi ‘The animal of Calderon-Diego Costa’.

Diego Costa alizaliwa na kukulia Brazil, aliondoka kwenda Ulaya akiwa na miaka 17. Hadi hayo maneno yakitoka katika kinywa cha Scholari, Costa alishaichezea Brazil mara mbili.

Diego Costa
Diego Costa

Wakati Brazil wanafikiria kuunda timu inayomzunguka Costa, Hispania walipita mlango wa uani na kumuwekea Diego ‘cheki’ juu ya meza yenye thamani ya kununua kisiwa chochote Hispania.

Costa alibadilisha mawazo ndani ya dakika mbili na kuamua kulikana taifa lake, akachagua kuitumikia Hispania. Mpaka leo wabrazil wanamuita ‘The Traitor’. Lakini Diego yeye hajali! Tayari pesa ilishasoma kwenye akaunti yake.

Baada ya Lorenzo Sanz kuiteka mioyo ya mashabiki wa Real Madrid, alikuwa na hakika kwamba anakwenda kushinda urais kwa mara nyingine. Ghafla alitokea Fiorentino Perez kusikojulikana kumpa changamoto.

Perez aliahidi kumshusha Luis Figo Real Madrid iwapo atashinda urais. Watu walimuona Perez kichaa asiye na jalala, Luis Figo aliyekuwa mchezaji bora wa dunia anayekipiga Barcelona anawezaje kusajiliwa na Real Madrid? Ila Perez alikuwa na mahesabu yake. Aliahidi kuwalipia viingilio vya msimu mzima mashabiki wa Real Madrid iwapo kama atakuwa rais na kushindwa kumsajili Figo.

Luis Figo
Luis Figo

Perez alikuwa na mahesabu yake, alishamuweka Figo kwenye mtego wa pesa kabla hajatoa ahadi yake. Na kweli mwaka 2000, Perez alimshusha Figo Real Madrid. Barcelona hawakuamini macho yao. Mpaka leo pale Barcelona wanamuita Figo, Yuda Iskariote. Hadi waliwahi kumlenga na kichwa cha nguruwe.

Labda hizi stori zinaweza zisihusiane na picha iliyopostiwa na mwanadishi Nguli wa Habari za michezo bwana Deo Mwanasoka, Lakini wahenga wanasema Lisemwalo Lipo na Kama Halipo basi Linjiani.


UMEJARIBU HII POKER YA VIDEO?

Jaribu sasa hapa Meridianbet. Ukiacha ukweli kuwa itakupa burudani maridadi, bado inakuhakikishia ushindi mkubwa. Kazi kwako kukusanya ushindi!

Meridianbet Casino

INGIA MCHEZONI!

22 Komentara

    Bora tu chama abaki simba maana uko anakotaka kwenda hakumfai wala sio level yake chama kwenda yanga

    Jibu

    Ha ha ha tunasubiri muamuzi wa mwisho.yetu macho…Haji ataambia nini watu

    Jibu

    Nice update

    Jibu

    Tunasubiri wakati ufike ndo tutaona Maamuzi yake Ni yapi kubaki au kusepa

    Jibu

    Maamuzi ni yake mwenyewe

    Jibu

    Chama ni mali ya Simba hao utopolo watuache

    Jibu

    Yanga wanataka walipize ya morrison tatizo mkwanja wanao

    Jibu

    Chama ndio mtu wa mwisho kutoa maamuzi wapi anahitaji kwenda hao wengine wanapiga upatu tu

    Jibu

    Mchezaji kama mchezaji yeye ndo mwenye maamuzi yakufanya na kuamua aende wapi,sasa chama yeye ndo ataamua wapi pa kwenda

    Jibu

    Uamuzi niwake

    Jibu

    Maamuzi anayo yeye asiumize watu vichwa

    Jibu

    Abaki tu simba

    Jibu

    Abaki tu simba yanga hatuna shida nae

    Jibu

    uamuzi ni wake

    Jibu

    Asnt kwa taarif meridianbet

    Jibu

    Uwamuzi ni wake kwenda yanga au kubaki mana yeye ndio anae yuwa wapi aende

    Jibu

    Nice

    Jibu

    Chama ni mmoja tu

    Jibu

    Maneno hayo hayo yalisikika kwa Morrison kwenda simba kila mchezaji hana nafasi yake ya kuchagua sehemu sahihi hapa tunasubiri kuona mahamuzi yake chama

    Jibu

    Hapo ni maamuzi yake kubaki kuendeleah Simba au kwenda utopolo fc

    Jibu

    Chama asipokua makin na hiv vilabu vitamuulia soka lake mapema kama akina kichuya

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.