Klabu ya Barcelona imeripotiwa iko mbioni kumshtaki nyota wake wa Zamani Neymar kwa kile wanachokiita ni kumzidishia malipo kwa zaidi ya Euro milioni 9 alipokuwa Barcelona.
Inakumbukwa nyota huyu wa PSG tayari alishalazimishwa kurejesha takribani Euro milioni 5.9 ambazo pia zilionekana kuwa ishu kwenye masuala ya bonasi.
Hata hivyo, kwa mujibu wa The Sun, Barcelona walifanya hesabu vibaya za makadirio ya malipo ya Neymar na Kodi kwa miaka miwili ya awali na kujikuta wakilipa zaidi ya ilivyotakiwa.
Taarifa zaidi zinaripoti Wakala wa Kodi wa Barcelona tayari wametoa neno kwa Barcelona kuwa ikiwa watashindwa kufikia muafaka suala hilo, basi €9m itachukuliwa kama ni pesa ‘waliyojitolea kwa Neymar’ kama zawadi tu.
Huu ni muendelezo wa migogoro iliyoripotiwa kati ya pande hizi mbili. Mwezi Januari, Neymar aliripotiwa kuwa yeye ndiye anawashtaki Barcelona kwa takribani €3m – ambazo ni sehemu ya mshahara wake ambayo haijalipwa.
Baadala yake, taarifa mpya zinawataja Barcelona wakitaka kurejesha mara tatu ya pesa ambayo Staa huyu alitajwa kudai.
Sakata hili kwa upana wake linaihusisha na klabu ya Santos, ambayo Neymar aliondoka kuelekea Barcelona. Sekeseke hili pia halimuachi salama aliyekuwa raisi wa Barcelona Josep Maria Bartomeu anayeshutumiwa kwa udanganyifu wa kodi na rushwa.
Suala hili linaibuka wakati Barcelona wakiwa wanajaribu kuweka sawa vitabu vyao vya fedha baada ya kupata changamoto kubwa ya kiuchumi kutokana na janga la Corona.
Jaribu sasa hapa Meridianbet. Ukiacha ukweli kuwa itakupa burudani maridadi, bado inakuhakikishia ushindi mkubwa. Kazi kwako kukusanya ushindi!



Tatu
Barcelona waache ubabaifu walipe tu kumaliza kesi
Dorophina
Barca wanayumba kama makosa waliyafanya ni wao wenyewe kwaiyo ni kazi bure kumshtaki neymar
Elika
Barcelona sasa wanafika mbali sana..wakae wayajenge
Fatina mfigi
Duh mambo yamefikia uko mbon htr kwa neymar
Magdalena
Barcelona Hawana haja ya kumshitaki sababu kama makosa waliyafanya wenyewe yeye hakuiba
Fatuma kasomo
Gud news
Khadija
Inakuwaje sasa kwa upande wa neymar
Saupha mohamed
Hawamfanyii khaki kabsaa wamalizane tu
Angelina
Nice update
Mwajumah
Barcelona walipo fika sio pow bora wakae tu wayajenge
Carolyn
Swala la pesa kwa Neymar sio tatizo.ni kitendo cha kukaa mezani na kuyamaliza
Sabrina
Duuh ndio yamekua hayooo
felister
wamalizane tu jamaniii
Janeflora malisa
Asnt kwa taarif
Ester jackson
Barcelona mmepotea sasa mnaaza sababu nyingine tu hizo zisizo na mashiko siku zote hizo mlikuwa wapi hasaivi ndio mnamuona yuko vizuri ndio mana mnaingiza maneno yenu muacheni nerymaa ale good time yake vema
Rahma
Nice
Shani
Neymar ni malipo yasiyo hak kwa timu yk
Saupha mohamed
Good news
Zeiyana
Hiyo wafanye tu kama bonus zake kipindi alichokupo clabuni hapo wasitengeneze chuki na wachezaji hitajenga twasira mbaya kwenye clabu yao
Povel
Nice information
Issa
Neymar ni mwanzo tu ila barca itamuandam sna kwa sababu ilitumia gharama nying pasipo kufaidika nae