Klabu ya Simba sc imethibitisha kuongeza mikataba ya wachezaji wake wawili muhimu, beki wa kati Rushine De Reuck na kiungo mkabaji Yusuph Kagoma, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha kikosi cha timu hiyo kwa misimu huu na ijayo.
Kwa mujibu wa taarifa ya klabu ya simba, beki huyo raia wa South Africa, Rushine De Reuck (30), amesaini nyongeza ya mkataba mpya wa mwaka mmoja utakaomuweka ndani ya klabu hiyo hadi mwaka 2027. Nahodha huyo mpya wa Simba alijiunga na timu hiyo akitokea Mamelodi Sundowns, na mkataba wake wa awali ulikuwa unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu kabla ya kuongezewa.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Wakati huohuo, kiungo mkabaji wa Simba Yusuph Kagoma naye ameongeza mkataba mpya wa miaka miwili ambao utamuweka kuendelea kuitumikia Simba Sc hadi mwaka 2028, hatua inayoonesha imani ya klabu hiyo kwa mchango wa wachezaji hao katika kuimarisha kikosi cha Msimbazi.


