Mjumbe Mwingine wa Simba Aibuka na Mapya.

BADO sakata la mgogoro ndani ya Uongozi wa Simba linaendelea, mapya yameibuka tena moja ya wajumbe upande wa Wanachama sha Baraka ameibuka na kusema kwamba hiki ni kipindi cha mpito. Jisajili Merdianbet ili uwe sehemu ya washindi wa kila siku.

Asha Baraka amewataka mashabiki wa Simba kuwa na utuluvu huku akisisitiza kwamba hali hii inayoendelea katika klabu yao itapita, hata vilabu vya Ulaya na timu nyingi za Mpiria hupitia haya.

Akizungumza na Wasafi FM mapema asubuhi ya Leo Asha Baraka amekuwa mpole na kuchagua kukaa kimya kwa upande, huku akisikiliza wakubwa zake watasemaje, akimaanisha Salim Abdallah Try Again, na Mwenyekiti wa Simba Murtaza Mangungu. Cheza na Ushinde mamilioni kupitia Meridianbet kasino ya mtandaoni.

“Mimi ni mmoja wa bodi ya wakurungenzi kwa muda mrefu, ngoja tuwasikilize wajumbe wanasemaje, tuna wakubwa zetu Mwenyekiti wa klabu, Mangungu, Try Again watasema”

“Hivi vitu ni vya muda tu, vitaisha Simba haiwezi kuwaka moto muda wote tu, ngoja tumsikilize na Mwekezaji anasemaje kwenye hili, hiki ni kipindi cha mpito tu kitapita, hata Liverpool na Manchester Utd walishapitia haya” Asha Baraka Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi upande wa Wanachama.

Wiki iliyopita Baadhi ya Wajumbe wa Wanachama wakiongozwa na CPA Issa Masoud walifanya kikao, na kuzungumzia sakata zima la mgogoro uliopo kati ya wao na Muwekezaji wa timu hiyo Mohammed Dewji “MO”

Baada ya kikao hicho yaliibuka maswali kutoka kwa mashabiki na wanachama wakiushutumu uamuzi na kulaani kile kilichozungumzwa, kwenye kikao hicho ambapo Viongozi hao walisisitiza kwamba hawatojiuzulu kwa sababu wao hawana shida, mwenye shida ni muwekezaji. Ushindi ni sehemu ya maisha Meridianbet, kuwa familia ya mabingwa kwa kubashiri michezo kwa odds kubwa na kucheza kasino ya mtandaoni na michezo ya sloti hapa.

Acha ujumbe