Simba Yashusha Chuma Kipya

SIMBA

Baada ya kuukosa ubingwa wa Ligi kuu bara, Simba SC imeanza kujiandaa na msimu ujao haswa katika upande wausajili wa wachezaji wapya. Tembelea duka la ubashiri-Meridianbet kutandika jamvi lako kwa odds kubwa.

Uongozi wa Simba umefikia maamuzi ya kumtambulisha Mkuu wa Scouting Mels Daalder,  mwenye uwezo wa kutathimi soka na wachezaji. Beti na Meridianbet kwa odds kubwa na machaguo kibao, pia unaweza kubashiri mubashara.

Taarifa kutoka klabu hiyo iliandika “Klabu ya Simba Sports Club imemteua Mels Daalder kuwa skauti wake Mkuu. Mels ni raia wa Uholanzi mwenye uzoefu wa kufanya skauti kwenye timu mbalimbali.

“Mels ameshiriki kozi mbalimbali za Scouting duniani ikiwa ni pamoja na kozi zikizoendeshwa na skauti wa zamani wa Manchester United, David Hobson.”

“Mels ambaye ameshawahi kuishi Tanzania, ni shabiki mkubwa wa Simba pia ni mjuzi wa kufanya upembuzi (analysis) na ana ujuzi mkubwa na ufahamu mkubwa wa ligi ya Tanzania, Afrika Mashariki na Afrika.”

“Mels anaongea lugha kadhaa ikiwemo; Kiholanzi, Kiingereza, Kijerumani, Kifaransa na Kiswahili kwa kiasi fulani.”

Akizungumza juu ya uteuzi wa Mels; Afisa Mtendaji Mkuu wa Simba Sports Club Imani Kajula amesema ” Tunafuraha kubwa kumkaribisha Mels ili kuja kuboresha ufanisi kwenye scouting kwani ni eneo muhimu sana kwenye mafanikio ya klabu yetu. Tunaendelea na maboresho muhimu kuelekea msimu mpya wa ligi na mashindano ya kimataifa”.

Eneo la usajili la Simba kwa misimu miwili limeshindwa kufanya kazi yake, kwani iliwasajili wachezaji ambao walishindwa kuipata timu hiyo matokeo yake, usajili wa wachezaji kama Pape Osmane Sakho, Peter Banda, Ismael Sawadogo, Nelson Okwa, Augustine Okrah n.k ni usajili wa wachezaji wa kigeni ambao hawajaonesha uwezo wa kutisha sana. Ukiwa na Meridianbet unapata odds kubwa, kasino ya mtandaoni na michezo ya sloti.

Kuelekea msimu ujao 2023/24 huenda Simba wakawa wamefanya chaguo sahihi. Pata odds kubwa kutoka Meridianbet kwa mechi za ligi mbalimbali.

Acha ujumbe