Ikiwa ni miezi miwili tu imeisha toka aliposajiliwa na klabu ya Reading, Andy Carroll ameondoka klabuni hapo na kutua West Bromwich Albion kwa miezi 6 ijayo.
Carroll anajiunga na timu hiyo baada ya mshambuliaji wake, Daryl Dike kupata majeruhi ya paja na atakuwa nje ya uwanja kwa muda.
Usajili wa Andy Carroll unakwenda kuongeza nguvu kwenye safu ya ushambuliaji wakati huu ambao, West Bromwich Albion wanapambana kupanda daraja ili wacheze EPL msimu ujao.

Carroll aliwahi kucheza kwenye vilabu vikubwa kama vile Liverpool, Newcastle na West Ham ikiwa ni sambamba na kuitumikia Timu ya Taifa ya Uingereza.
Dakika tano pekee zinakutosha kuwa mmoja wa washindi wa mkwanja mrefu ndani ya kasino pendwa ya meridianbettz katika sloti maridhawa ya KENO, moja ya michezo inayoipa thamani dau lako.


