Panapofuka moshi, moto unawaka. Hii ndio hali halisi kuelekea ufunguzi wa dirisha la usajili majira ya joto. Bayern Munich watafanikiwa kwa Saidio Mane?
Maongezi ya mkataba mpya kati ya Mane na Liverpool hayaoneshi kuzaa matunda, hii ni baada ya klabu hiyo kuonekana ikimpa nafasi kubwa Mo Salah kuliko swahiba wake, Mane. Hata hivyo, hata mkataba mpya wa Salah bado ni kizungumkuti, makubaliano hayafikiwi kwa muda sasa.
Wakati Liver wakiendelea kujitutumua, Bayern Munich hawa hapa. Wanaingia miguu yote kwa Saidio Mane wakiwa na lengo la kumtoa Anfield na kumpeleka Alianz Arena kule Ujerumani.
Inaripotiwa kuwa, wikiendi hii, Mkurugenzi wa The Bavarians alikutana na wawakilishi wa Mane kwa ajili ya mazungumzo ili kuweka sawa mipango ya kumsajili mchezaji huyo mwishoni mwa msimu huu.
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.