Baada ya kushuhudia ofa mbili kukataliwa na Brighton, hatimaye Arsenal wamejiongeza kwa Ben White na sasa uwezekano wa kumsajili ni mkubwa.
Dau la mwisho la Arsenal (kabla ya kuongeza dau) lilikuwa £47M ambapo Brighton Hove Albion walilikataa mchana kweupe. Arteta akaona isiwe tabu, sasa ni rasmi wanamchukua Ben White kwa dau la £50M.
Japokuwa vilabu vimekubaliana dau lililotolewa, usajili wa White utafanyiwa kazi vizuri atakaporejea kutoka likizo – Julai 26,2021 ambapo atafanyiwa vipimo vya afya sambamba na taratibu zingine za kukamilisha usajili huo.

Mpaka sasa, Arsenal wameshamsajili Nuno Taveres, Sambi Lokonga (anasubiri kukamilisha usajili baada ya kukaa karantini) na White atakua n mchezaji wa tatu kutua Emirate. Hakika Arteta hatanii kuelekea msimu ujao.
Ndio, kama bado hujajiunga na Familia ya Mabingwa ya Meridianbet, huu ndio wakati wako! Tunakupatia Bonasi ya 3,500 Tsh papo hapo kama sehemu ya ukaribisho!


