Brahim Diaz yuko mbioni kujiunga tena na AC Milan kutoka Real Madrid kwa mkataba wa mkopo wa miaka miwili. Mchezaji huyo atawasili Italia wikiendi hii na kukutana na timu ya Stefano Pioli, ambaye tayari alicheza kwa mkopo msimu uliyopita.

Hii inaweza kuwa hatua nzuri kwa AC Milan na Real Madrid, na pia kwa mchezaji.
Hapa, tunaangalia jinsi hii inavyofaidi pande zote.
Mchezaji
Brahim ndiye mhusika mkuu na ndiye anayefaidika zaidi. Atapata dakika katika timu bora na pia atachukua jezi namba 10 ambalo Hakhan Calhanoglu alikuwa akivaa.
Rossoneri wanamwamini Brahim na hilo ndilo jambo la kwanza kijana huyo kutoka Malaga alitaka kujua.

AC Milan
Klabu ilipata kile walichotaka. Pioli anamwamini na walimpata Brahim kwa ada kidogo.
Wana miaka miwili kukomaa kwa mchezaji ambaye anaweza kuleta furaha kwa timu kurudi kwenye Ligi ya Mabingwa.
Real Madrid
Real Madrid itapokea karibu euro milioni nne kwa mkopo huo. Wakati bado hawajapata kile walicholipa kwa Brahim – ambayo ilikuwa euro 17m – hawatampoteza mchezaji huyo.
Los Blancos pia wana fursa ya kumrudisha baada ya msimu kama walivyofanya kwa Martin Odegaard.
Ndio, kama bado hujajiunga na Familia ya Mabingwa ya Meridianbet, huu ndio wakati wako! Tunakupatia Bonasi ya 3,500 Tsh papo hapo kama sehemu ya ukaribisho!


