Kocha Slaven Bilic wa West Bromwich Albion amesisitiza kwamba “sijafanya kosa lolote” licha ya kukubali kutozwa faini ya Bilic Apigwa Faini ya £8,000 kutoka kwa Shirikisho la Soka la Uingereza (FA).
Mkufunzi huyo raia wa Croatia alionyeshwa kadi nyekundu mwishoni mwa kipindi cha kwanza katika mechi iliyokutanisha kikosi chake na Everton kwenye Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) mnamo Septemba 20, 2020.

Chini ya kocha Carlo Ancelotti, Everton walisajili ushindi wa 5-2 katika mechi hiyo iliyochezewa uwanjani Goodison Park.
“Nilizungumza na viongozi wa FA na wasimamizi wa klabu ya West Brom baada ya mechi hiyo. Licha ya kuwasisitizia kwamba hakuna kosa nililokuwa nimefanya, bado nilitakiwa kulipa faini,” alitanguliza bilic.
“Ingawa sikubaliani kabisa na maamuzi hayo, nimekubali faini kwa sababu ndiyo njia rahisi zaidi ya kuondokea balaa, Kusahau yaliyojiri na kuendelea mbele na majukumu yaliyopo mbele yetu,” akasema kocha huyo.

Bilic, 52, aliambulia kipigo Goodison na kuanza kumzomea refa Mike Dean aliyemwadhibu beki wa zamani wa Arsenal, Kieran Gibbs kwa kumkabili vibaya fowadi mpya wa Everton, James Rodriguez aliyeagana na Real Madrid mwanzoni mwa mwezi huu.
West Brom watakuwa wenyeji wa Chelsea uwanjani The Hawthorns mnamo Septemba 27, 2020, na Bilic ambaye hakupigwa marufuku, ataruhusiwa kukaa katika sehemu ya makocha baada ya kutozwa faini.
FURAHIA KASINO YA MTANDAONI
Tembelea ardhi ya maajabu ushangazwe na mengi ikiwa ni pamoja na urahisi wa kujipatia utajiri kupitia Kasino ya Meridianbet.


magdalena
alipe tu faini hakuna namna maana kashaandikiwa makosa tayari
Mwajumah
Duuh majanga ayo yamemkuta Bilic ila ndio Mambo ya kimichezo yalivyo
sylvester
Kocha huyu wa West brown Slaven Bilic sidhani kama kulikua na uhitaji wa kutozwa faini ila kadi nyekundu alistahili,kocha kama kocha akiona anatendewa sivyo basi yupo na haki ya kuhamaki na ile ilikua hamaki tu,ila wakulungwa FA ndio washamtwanga fine hivyo
Adelta
Aende tu akalipe fine ili mambo yaishe
Tatu
Kukubali kosa sio kutenda kosa bora ya kukubali yaishe mambo mengine yaendelee
Lydia Emmanuel Magoti
Duu alipe tuu fain akuna jinsi ndio ivyo ishatokea ndokashandikiwa kosa akunajinsi
Dorophina
Alipe tu ili yasiwe Mambo mengi
Caroline
Pole yao
Sauda
Du! Pole yake..
Shan
Pole yake
Zeiyana
Kama sheria ndio ilivyo bac hanaaki ya kutozwa faini
Khadija
Alipe tu fain mana hakuna namna
Sadick
Kuna kitu kinatengenezwa kwenye mpira ambapo maamuzi mabaya ya marefa hayahojiwi na yeyote na mwisho siku watabaki kuwa miungu watu ktk mchezo wa mpira wa miguu#meridianbettz
Venerose
Alipe tu faini ili iwe fundisho kwa wengine
Janeflora malisa
Pol yk
Juliana
Jamani
Genia Sikaluzwe
Pole yake
aisha
Duuh pole sana bilic kila kazi inachangamoto zake hata kama wewe mwenyewe unajua kuwa hujafanya kosa lakini shelia imesema hivyo basi lipa tuu kwani kila tatizo linalokuyokea mwanadam huwa linakuaga limebeba mbegu ya suluhisho
Fatuma kasomo
Duh polee
Samiah
Pole sanaaa
Rose kapinga
Alipe tuu mambo yasiwe mengi!!!
Issa
Adhabu inastahil kwa mtu kam huyu ambae ni mwalim anefundisha anatakiwa awe kiongoz bora
Elika
Haina namna ilipwe tu kiroho safi
Hopemwaikuka
Lipa tu baba hakuna jinsi
Rehema
Pole sana
Marry Mushi
alipe na abadilike
Gabriel
kutozwa faini ila kadi nyekundu alistahili,kocha kama kocha akiona anatendewa sivyo basi yupo na haki ya kuhamaki na ile ilikua hamaki tu,ila wakulungwa FA ndio washamtwanga fine hivyo
Frank P
Hakuna namna lkn alikuwa anajaribu kuexpress kuhusu maamuzi yasiyo sahihi katika mchezo
Ernest
Ajali kazini ajipange upya tuu
Tumaini kasalile
Duuh pole yake
Ester jackson
Duuh alipe tu mana mda mwengine marefa pia wanakosea sema tu likitokea uwanjani refa ndio mwamuzi wa mwisho
Sabrina
Duuh hatari alipe tu hakuna jinsi
Neema
Pole yake. Ila hana jinsi alipe tu mambo yasiwe mengi
Fatina mfingi
Pole
felister
majanga
Saupha mohamed
Pole sana
Amiri Kayera
Duh
David Pere
Kuna kitu kinatengenezwa kwenye mpira ambapo maamuzi mabaya ya marefa hayahojiwi na yeyote na mwisho siku watabaki kuwa miungu watu ktk mchezo wa mpira wa miguu
Povel
Duh majAnga kwl