Nahodha wa Simba SC John Bocco ameeleza kuwa mashabiki wa Simba wanacheza sehemu kubwa ya kuwatengeneza kisaikolojia hata pale wanapokuwa wamepoteza mchezo.
“Kitu wanachofanya mashabiki wa Simba [kiwapigia makofi wachezaji licha ya kupoteza mechi] ni kitu kikubwa sana.
Wao wanaweza wasijue inamaana gani kwetu lakini huwa wanatupa mtihani mkubwa, umepoteza mechi halafu unashangiliwa. Utaona mashabiki wa Simba ni watu wa aina gani, tumepoteza lakini bado wapo na sisi, inatia sana moyo na kuwapa nguvu wachezaji ili kufanya vizuri kwenye michezo inayofuata.
Tunawaheshimu sana. Unajua huwezi kucheza mpira bila kupoteza au kwa kiwango cha juu siku zote”.
Maneno hayo aliyasema Bocco akizungumza na waandishi wa habari katika kipindi cha Sports Xtra cha Clouds TV.
Bocco pia alieleza kuwa bado anadaiwa na mashabiki hao wa Simba kwani bado anaamini anataka kucheza nusu fainali au fainali ya kombe la mabingwa Afrika.
Ndio, kama bado hujajiunga na Familia ya Mabingwa ya Meridianbet, huu ndio wakati wako! Tunakupatia Bonasi ya 3,500 Tsh papo hapo kama sehemu ya ukaribisho!



Sadick
Hivyo ndivyo wanavyotakiwa kufanya wapenzi wa kweli wa Simba na mchezo wa mpira wa miguu kwa ujumla wake. Mashabiki maandazi ni wa msimu huwa wa kitambo tu tena wakati wa Neema