Beki kisiki wa Lille, Sven Botman, anavichachafya vilabu vinavyowania sahihi yake. Kuna kazi ya ziada kumtoa Ufaransa.
Newcastle United na AC Milan ni vilabu viwili vinavyohusishwa zaidi na Botman katika dirisha hili la usajili. Kwa hali ilivyo, Lille wanaweka ugumu kwa usajili huu kufanyika. Milan wameanza kuamini kuwa, huu ni mpango wa Lille kutotaka kuachana na mchezaji huyo ambaye amewekewa thamani ya £41M.
Inasemekana, Milan wameamua kujiondoa kwenye mchakato wa kumsajili beki huyu na, badala yake, viongozi wa Milan wanahamishia majeshi kwenye timu ya PSG wakimsaka Abdou Diallo.
Hata Diallo hatopatikana kirahisi, PSG wameweka thamani ya £16.7M. Milan wanataka kutumia mfumo waliotumia kumtoa Fikayo Tomori kule Stamford Bridge. Wanamuhitaji Diallo kwa mkataba wa mkopo ambao utakuwa na kipengele cha kumsajili moja kwa moja mwishoni mwa msimu.
Kwa Botman, wamebaki Newcastle United pekee. Watafanikiwa kumtoa Lille au wataamua kuchukua uamuzi kama wa AC Milan?
Ni muda wako kujiachia na mchezo maridhawa wa Almighty Aztec katika kasino bomba za meridianbettz. Nafasi ya kutengeneza mkwanja iko mikononi mwako kazi ni kwako.

CHEZA HAPA

