Klabu ya Chelsea na Liverpool wanaripotiwa kumtaka kiungo wa AC Milan Ismael Bennacer, ambaye huenda akapatikana mwishoni mwa msimu huu.
Kiungoo huyo mwenye miaka 24, aliitumikia akademi ya Arsenal kabla ya kuelekea Empoli, ambako alivutia timu nyingi kutokana na ubora wake kiasi cha kununuliwa kwa Euro milioni 16 kwenda Milan mwaka 2019.
Bennacer ana mechi 42 za Kimataifa za Algeria baada ya kucheza kwa mara ya kwanza akiwa na umri wa miaka 18, na ameanza katika mechi saba kati ya nane za Serie A za Milan kuanza kampeni hii, lakini hali ya mkataba wake inaweza kuharakisha kuondoka kwake Italia.
Mkataba wa Mchezaji huyo unamalizika 2024, mwishoni mwa msimu ujao, lakini kadiri muda unavyosonga kabla ya kusaini mkataba wa nyongeza, ndivyo Milan watakavyokuwa na shinikizo kubwa la kutaka pesa taslimu badala ya kumwacha aondoke bure.
Kulingana na Calciomercato, Milan wanamthamini Bennacer kwa Euro milioni 50 huku Chelsea, Liverpool na wapinzani wao wa Serie A Juventus wakifuatilia kwa karibu maendeleo yake. Ripoti inasema kumwondoa Milan mnamo Januari kunaweza kuchukua “ofa ya kupendeza”, lakini ikiwa Milan itaamua kuona msimu uliosalia nguvu yao katika mazungumzo itakuwa dhaifu sana.
Bennacer na mchezaji mwenza Rafael Leao wanavutiwa na vilabu vikubwa Chelsea ikiwa ni mojawapo na Milan haitakuwa na bajeti ya kuongeza nyongeza mbili kubwa.